Familia BORA

Familia BORA Ubora katika familia ni chanzo kikubwa cha maendeleo binafsi na katika jamii inayoizunguka.

Afya ni kuwa na hali nzuri kimwili, kiakili, kijamii, kiroho, kiutu na kisaikolojia bila kusumbuliwa na ugonjwa wowote. ...
28/02/2024

Afya ni kuwa na hali nzuri kimwili, kiakili, kijamii, kiroho, kiutu na kisaikolojia bila kusumbuliwa na ugonjwa wowote.
Kulingana na WHO (World Health Organization – Shirika la Afya Duniani) Afya ni hali ya ustawi kamili wa kimwili, kiakili na kijamii. Sio tu ukosefu wa magonjwa au udhaifu.
Afya njema ni njia ya afya ambayo inasisitiza uzuiaji wa magonjwa na kuongeza muda wa maisha kinyume na kusisitiza kutibu magonjwa
Ili kuwa na afya bora ni vyema kuzingatia kanuni na taratibu bora za afya. K**a mlo kamili (kukiwemo na virutubisho vyote vya chakula), usafi wa mwili, usafi wa mazingira na kuwa na afya ya kiroho (kuishi kwa mapenzi ya Mungu k**a kupendana, kuthaminiana na kuacha dhambi.)
Ipende afya yako na vilevile jali afya ya familia yako. Itawasaidia kuepukana na magonjwa.

Chakula na huduma kwa wazee. Wazee wanapotumia lishe yenye afya na uwiano wana uwezekano wa kuwa na afya bora na kufanya...
25/07/2022

Chakula na huduma kwa wazee.

Wazee wanapotumia lishe yenye afya na uwiano wana uwezekano wa kuwa na afya bora na kufanya kazi kwa mda mrefu. Kwa kutumia mlo sahihi huwawezesha kuwa na afya njema na wenye nguvu wakati wote na kwa mda mrefu.
Mahitaji ya nishati ya wazee kwa kawaida huwa chini ya yale ya vijana lakini wanahitaji angalau kiasi sawa cha protini na virutubishi vidogo vidogo.

MATOKEO YA KUTOKULA VIZURI Watu hula chakula kingi (haswa vyakula vyenye nguvu nyingi na vyenye mafuta mengi) kuliko wan...
14/06/2021

MATOKEO YA KUTOKULA VIZURI

Watu hula chakula kingi (haswa vyakula vyenye nguvu nyingi na vyenye mafuta mengi) kuliko wanavyohitaji. Kwa kutumia chakula chenye nguvu nyingi na mafuta mengi hupelekea mwili kunenepa kupita kiasi.

Watu hawa wako katika hatari kubwa ya magonjwa sugu, k**a ugonjwa wa moyo, shinikizo la damu na ugonjwa wa kisukari.

Utapiamlo (hutokana na kutopata virutubisho vya kutosha au kupata virutubisho vingi / vya ziada na kupelekea matatizo katika afya ya mtu husika) ni moja wapo ya shida kubwa za kiafya ulimwenguni.

• Zaidi ya nusu ya vifo vya watoto wenye umri wa miaka 0-5 vinahusishwa na utapiamlo.
• Katika nchi nyingi theluthi moja ya watoto wadogo wamedumaa na asilimia 10 ni wembamba (kukondeana kutokana na utapiamlo).
• Takriban theluthi ya watoto wachanga wana uzito mdogo wa kuzaliwa, ambayo inawafanya waweze kuugua, kukua polepole na kufa.
• Upungufu wa damu unaosababishwa na ukosefu wa chuma ndio shida kubwa ya lishe. Katika maeneo mengi nusu ya wanawake wana upungufu wa damu.
• Upungufu wa Vitamini A, iodini na zinki imeenea katika nchi nyingi.
• Uzito / unene kupita kiasi na shida zinazohusiana nazo zinaongezeka katika nchi nyingi

MATOKEO YA KUTOKULA VIZURI Watu wengi hula chakula ambacho hakina usawa (unbalance diet) na chenye virutubisho vichache....
07/06/2021

MATOKEO YA KUTOKULA VIZURI

Watu wengi hula chakula ambacho hakina usawa (unbalance diet) na chenye virutubisho vichache. Ni nini matokeo yake ukiwa hufuati usawa katika chakula:

• Ikiwa kuna ukosefu wa madini chuma, ukuaji wa akili na mwili wa watoto unaweza kucheleweshwa. Watu wa rika tofauti huwa hawajishughulishi sana na wana kinga ndogo inayopelekea maambukizo na wanaweza kupata upungufu wa damu.
Upungufu wa damu kwa wanawake wajawazito ni hatari kubwa sana na isipozingatiwa husababisha vifo wakati na baada ya ujauzito.

• Ikiwa kuna ukosefu wa iodini, watu huwa na desturi ya kutokujali na hupata shida kufanya kazi au kusoma. Wakati mwingine hupelekea ukuaji wa goitre. Mwanamke ambaye hana iodini katika kipindi cha mapema ya ujauzito wake yuko katika hatari kubwa ya kupata mtoto ambaye atahathirika kiakili na kimwili. Kwa mfano, mtoto anaweza kuwa na IQ ya chini au kuwa kiziwi.

• Ikiwa kuna ukosefu wa vitamini A, watu wana uwezekano wa kuugua kwa sababu ya upungufu wa kinga ya mwili. Kuwa na upungufu mkubwa wa vitamini A, husababisha hali ya macho ambayo hutoka kwenye upofu wa usiku hadi macho kavu (xerophthalmia), hadi uharibifu wa koni na upofu. Hali hizi za macho hufanyika mara nyingi kwa watoto wadogo na wanawake wajawazito.

Zingatia kula chakula chenye virutubisho vya usawa kwa ajili yako na ya familia yako.

UTAPIAMLO NI NINI?Utapiamlo ni hali ambayo hutokana na kutopata virutubisho vya kutosha au kupata virutubisho vingi / vy...
31/05/2021

UTAPIAMLO NI NINI?

Utapiamlo ni hali ambayo hutokana na kutopata virutubisho vya kutosha au kupata virutubisho vingi / vya ziada na kupelekea matatizo katika afya ya mtu husika.

Kwa asilimia kubwa utapiamlo umesababishwa na ukosefu wa lishe, ambayo ni ukosefu wa kalori, protini, mafuta, wanga, vitamini na madini mwilini vilivile husababishwa na kupata lishe nyingi sana mwilini.

Mahitaji ya mwili na ulaji wa virutubisho ni vya muhimu sana kwa watoto, vijana, wazee na wanawake wajawazito. Hivyo ni muhimu kuzingatia ulaji wa chakula kwa usawa.

Marasmus – ni utapiamlo unaosababisha uzito wa mtoto kuwa chini sana kwa umri wao. Ambayo husababishwa na ukosefu wa vir...
25/05/2021

Marasmus – ni utapiamlo unaosababisha uzito wa mtoto kuwa chini sana kwa umri wao. Ambayo husababishwa na ukosefu wa virutubisho, hutokea kwa watoto ambao hawapati protini za kutosha, kalori, wanga, na virutubisho vingine muhimu. Hii kawaida husababishwa na umaskini na uhaba wa chakula

Kwashiorkor ni lishe duni inayotokea kwa sababu ya upungufu wa protini. Kwashiorkor ni hali mbaya ambayo inaweza kutokea wakati mtu hatumii protini ya kutosha. Ukosefu mkubwa wa protini unaweza kusababisha uhifadhi wa maji, ambayo inaweza kufanya tumbo kuonekana limevimba.

MATOKEO YA KUTOKULA VIZURIWatoto na watu wazima wanapokula chakula kidogo au kisichowatosheleza hupelekea kupata utapiam...
18/05/2021

MATOKEO YA KUTOKULA VIZURI

Watoto na watu wazima wanapokula chakula kidogo au kisichowatosheleza hupelekea kupata utapiamlo kwa sababu wanakuwa hawajapata chakula cha kutosha au hawana hamu ya kula chakula.

Watu hawa hukosa nguvu na virutubisho vingi, ambapo husababisha:
• kuwa na nguvu kidogo kwa hivyo hawawezi kufanya kazi, kusoma au kucheza k**a kawaida
• kinga yao kuwa dhaifu na hupelekea kupatwa na magonjwa kwa urahisi
• watoto kutokukua vizuri na uzito wao kupungua. Ikiwa wanatumia chakula kidogo sana (mara nyingi hii hutokea wakiwa wamepata maambukuzi), mtoto anaweza kupata utapiamlo mkali (k**a. kwashiorkor au marasmus)
• kwa wanawake wajawizito ikiwa ana utapiamlo hupelekea mtoto wake ambaye hajazaliwa kukua vibaya.

MATOKEO YA KUTOKULA VIZURIWatu ambao wana lishe duni na hawali chakula chenye virutubishi na virutubisho sawa sawa mara ...
27/04/2021

MATOKEO YA KUTOKULA VIZURI

Watu ambao wana lishe duni na hawali chakula chenye virutubishi na virutubisho sawa sawa mara nyingi hupatwa na magonjwa na kuwa na utapiamlo. Aina ya utapiamlo ambayo hutokea, hutegemea na aina virutubisho, kiasi cha nishati inayotakiwa ya chakula kukosekana mwilini (au kuzidi) na hii pia hutegemea kwa muda gani imekosekana na umri wa mtu huyo.

Sumu na kemikaliChakula na maji inakuwa sio salama ikiwa ina sumu au kemikali hatari. • Sumu inayoitwa "sumu kuvu" imete...
02/04/2021

Sumu na kemikali
Chakula na maji inakuwa sio salama ikiwa ina sumu au kemikali hatari.
• Sumu inayoitwa "sumu kuvu" imetengenezwa na ukungu unaokua kwenye nafaka na jamii ya kunde. Kula sumu kuvu ni hatari sana na kunaweza kutufanya tuwe wagonjwa sana.

Namna ya kuzuia ukungu kukua kwenye chakula ni kwa kukausha mazao vizuri na kuyahifadhi mahali pakavu.

Usile vyakula vyenye ukungu. Usiwape wanyama

Dawa za wadudu na kemikali zingine hatari za kilimo zinaweza kuingia kwenye chakula au maji na kusababisha sumu ikiwa:
• kemikali haitumiwi kwa njia iliyopendekezwa
• vyombo vilivyokuwa wazi kuingia kemikali na kutumika kwa chakula au maji.

Nini cha kufanya.
• Fuata kwa uangalifu maagizo ya kutumia kemikali
• Kuwa mkali juu ya kuweka kemikali mbali na watoto
• kamwe usiweke chakula au maji kwenye vyombo ambavyo vimetumika kwa kemikali
• Nawa mikono baada ya kutumia kemikali, na safisha vyakula vyovyote (mfano matunda) ambavyo vimepuliziwa nazo.

Usafi katika mazingira ya nyumba.• Weka mazingira ya ndani na nje ya nyumba kwa usafi bila uchafu wa aina yoyote, safish...
26/03/2021

Usafi katika mazingira ya nyumba.

• Weka mazingira ya ndani na nje ya nyumba kwa usafi bila uchafu wa aina yoyote, safisha vinyesi vya wanyama na takataka zingine.
• Weka takataka kwenye p**a lililofunikwa na umwage kila mara ili isivutie nzi.
• Fundisha watoto kujali na kutunza usafi wa mazingira.

Uandaaji wa Chakula• Weka mahali/sehemu pa kuandaa chakula kwa usafi. • Tumia vyombo visafi na vilivyooshwa kwa uangalif...
15/03/2021

Uandaaji wa Chakula

• Weka mahali/sehemu pa kuandaa chakula kwa usafi.
• Tumia vyombo visafi na vilivyooshwa kwa uangalifu kuhifadhi, kuandaa, kuhudumia na wakati wa kula chakula.
• Andaa chakula kwenye meza/sehemu ambayo haina vumbi
• Safisha mboga mboga na matunda kwa kutumia maji safi.
•Zuia nyama iliyo mbichi (ya kuku,samaki, ng’ombe n.k) kugusana na vyakula vingine, kwani vyakula hivi vya wanyama huwa na vijidudu (germs). Osha sehemu/meza uliyotumia na zilizoguswa na vyakula hivi vibichi kwa maji ya moto na sabuni.
•Pika nyama (ya kuku, samaki, ngo’ombe n.k) vizuri. Nyama haipaswi kuwa na juisi nyekundu.
• Chemsha mayai na uhakikishe yameiva vizuri. Usile mayai mabichi au yaliyopasuka. Hasa kwa wanawake wajawazito.
• Chemsha maziwa vizuri kabla ya kuyatumia.

Kununua na kuhifadhi chakulaFunika vyakula ili viwe safi na salama• Nunua vyakula vyenye ubora na usafi. Angalia viashir...
09/03/2021

Kununua na kuhifadhi chakula

Funika vyakula ili viwe safi na salama
• Nunua vyakula vyenye ubora na usafi. Angalia viashiria vya chakula chenye ubora duni.
• Funika vyakula vibichi na vilivyopikwa ili kuvikinga na wadudu, mende, panya na vumbi.
• Hifadhi chakula ulichonunua (haswa vyakula kutoka kwa wanyama) na vyakula vilivyopikwa mahali pazuri, au kwenye jokofu ikiwa inapatikana.
• Weka vyakula vikavu k**a vile unga na jamii ya kunde mahali pakavu na salama kuepuka wadudu, panya na wadudu wa aina yoyote
• Epuka kuhifadhi vyakula vilivyobaki kwa zaidi ya masaa machache (isipokuwa kwenye jokofu). Ziweke kila wakati zikiwa zimefunikwa na pindi utaitumia tena zipashe moto vizuri hadi ichemke.

Address

Arusha

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Familia BORA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Familia BORA:

Share

Category