13/05/2020
VITA DHIDI YA UGONJWA WA COVID-19 NI YETU SOTE
Habari ndugu zangu,poleni na majukumu ya Kulijenga Taifa letu la Tanzania,,,
Sote tunajua kuwa tuna changamoto kubwa inayotukabili la Ugonjwa wa(CORONA) COVID-19 ambao kiukweli unahitaji umakini na Kila mmoja wetu kutekeleza maelekezo na miongozo yote jinsi ya kujikinga toka Wizara ya Afya lakini pia shirika la Afya duniani,,,jambo hili linahitaji team work linahitaji Mimi nitimize wajibu wangu na ww utimize wajibu wako ili sote tuwe salama,,,,
Nilibahatika wiki iliyopita kufika maeneo ya mpakani mwa Nchi yetu na Kenya eneo la NAMANGA ,na juzi,Jana na Leo maeneo ya Vijiji vya Tarafa ya Engaranaibo takribani kilometer 107 kutoka Arusha mjini,kilometer k**a 10 kuingia Nchi ya Kenya,eneo hilo lina vijiji zaid ya 11 vinavyochukulia huduma makao makuu ya Tarafa ya Engaranaibor yaani kata ya Engaranaibor pamoja na baadhi ya raia wa kigeni pia wapo maeneo hayo,ni eneo ambalo kuna mwingiliano mkubwa wa wananchi ikiwepo mnada wa Engaranaibor uliofanyika Jana ,mbali na shughuli kubwa kuwa ni ufugaji na kilimo wengi wa wananchi ambao wanazungumza lugha ya kinyumbani peke(Kimasai) uelewa juu ya ugonjwa wa corona bado ni mdogo sana,,,binafsi kwa kuona uhatari uliopo maeneo ya mipakani ili kuilinda Nchi yetu kwa wananchi wa maeneo hayo ya mipakani kuwa salama tulifika k**a MUNANTA MED CO.LTD kutoa elimu juu ya ugonjwa huu wa corona kwa viongozi wa vijiji vya Tarafa ya Engaranaibor,Viongozi wa Kimila ,Waganga wa Jadi,Wakunga jumla zaidi ya 71 na baadae wananchi waliohudhuria mnada wa Engaranaibor ikiwa ni mkakati mmoja wapo kusaidia kufikisha ujumbe wa serikali chini ya Wizara ya Afya juu ya mbinu za kujikinga na janga hili la Ugonjwa wa Corona,Pia tuliwapatia Barakoa 100,Ndoo za Kunawia mikono,na Sabani za kunawia Lita 65,,,
Mbali na Elimu hiyo ambayo ilifikishwa kwa kutafsiriwa kimasai pia Wakazi hao walielekezwa jinsi ya kunawa mikono kwa maji tiririka kwa maji safi na sabuni kwa muda wa sekunde ishirini na Zaidi ,jinsi ya kuvaa Barakoa na Maelekezo mengine ya kitaalamu ambazo pia zitaenda kusaidia taaisis za kidini k**a makanisa na misikiti na maeneo mengine ya mikusanyiko
Zoezi hili litakuwa endelevu nitoe wito kwa sote kuungana hasa kuzijali na kuzipatia elimu jamii zilizo kwenye hatari kubwa hasa maeneo yenye mikusanyiko na sana vijijini ambapo social media hazipo,vyombo vya habari havipo na wengi kipato chao ni cha chini na wengi hawajui hata kiswahili na vyombo vyote vya habari sidhani k**a kuna kinachowafikia kikizungumza kilugha chao cha nyumbani,,tunatajaria kufika kijiji cha KIMWATI ambacho ndio kijiji cha mwisho kuingia Kenya ambapo wananchi wake wanapata huduma za kiafya kituo cha afya ambacho tulichoambiwa kipo maeneo mpakani kabisa
ELIMU NI UFUNGUO WA KILA JAMBO,NILINDE NIKULINDE,NIKINGE NIKUKINGE
MUNGU IBARIKI TANZANIA🇹🇿🙏
Dr Juma A.Muna
CEO &FOUNDER-MUNANTA MED.CO.LTD
Visit us
Www.Munantamed.com