30/01/2022
SABABU zinazoweza kusababisha hedhi ya mwanamke kuchelewa, na nimefanya hivi kwa kutambua kwamba wanawake wengi hufikiria sababu moja tu endapo hedhi yao itakua imechelewa.
1 . Mimba
Hii ndio sababu ya kwanza kuja kichwani endapo siku za hedhi za mwanamke zitakua zimechelewa. Na inawezekana ukawa sahihi!! Na hii hutokea hata k**a mwanamke alishapata dalili zote za kwamba siku zake za hedhi ziko njiani, ila siku uliyotarajiwa ishuke inakua haishuki.
2 . Msongo wa mawazo.
Msongo wa mawazo huleta madhara katika mwili wa binadamu mara nyingi sana, mfano kuumwa kichwa, kuongezeka uzito, kuota vipele na hata vidonda vya tumbo, na k**a nilivyosema awali , k**a tayari umeshajua kwamba hedhi imechelewa msongo wa mawazo unaoupata kwa kufikiri sababu ni mimba ikiwa haukuwa umeitarajia unaweza kufanya mwili usiwe katika hali yake ya kawaida tena na hivyo kuendelea kusababisha kuchelewa kwa siku za hedhi zaidi na zaidi. Kwenye mwili wa mwanadamu kuna homoni mbili ziitwazo ‘adrenaline na cortisol’.
Hizi hufanya maamuzi kwenye mwili ya kipi kinaumuhimu zaidi ya kingine mpaka msongo wa mawazo utakapokuisha. Mara nyingi homini hizi huamua kuanza kazi katika vitu k**a msukumo wa damu na gesi mapafuni, huku kazi nyingine k**a mmeng’enyo wa chakula na mfumo wa kizazi kufuatia baadae na hivyo hata hedhi itachelewa kushuka k**a tatizo ndio hilo.
3 . Ugonjwa
Ugonjwa wowote unaweza sababisha hedhi kuchelewa kwa hedhi, hata k**a ni mafua au malaria. Ugonjwa uliona kwa wakati huo utakua ni kipaumbele cha kila homini mwilini mwako kuundoa k**a nilivyoelezea hapo juu kwa homoni zako kutoa kipaumbele kwa mifumo muhimu zaidi ya kizazi kwa wakati huo.
4 . Kubadilisha mazingira.
Kubadili mazingira kwa hapa naamaani chochote kile ulichokua unafanya zamani, ukakicha ghafla mfano ulikua unaishi sehemu ya baridi ukahamia yenye joto na kinyume chake, au kusafiri muda mrefu, k**a ulikua unafanya kazi usiku tu ukaanza kufanya kazi
KWA MAWASILIANO ZAIDI
☎️0656608552