03/06/2026
Akizungumza kupitia chaneli ya UTV, Azam Media, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Dkt. Peter Kisenge amebainisha kuwa mojawapo ya mambo wanayoyaona sasa ni kuongezeka kwa Wafanyakazi walioajiriwa ambao kazi zao zinahitaji kufikia kiwango fulani cha mafanikio (Key Perfomance Indicator-KPI's) ambao wanapata Madhara makubwa yatokanayo na Magonjwa yasiyo ya kuambukiza, hasa Presha.
Miongoni mwa Kinachosababisha changamoto hii ni Wafanyakazi hawa kuishi maisha yenye Stress pamoja na kukosa muda mzuri wa kupumzika ili watekeleze malengo waliyowekewa na taasisi zao.