Veriafya

Veriafya Taarifa sahihi za afya bila Upotoshaji! Kazi: [email protected]

03/06/2026

Akizungumza kupitia chaneli ya UTV, Azam Media, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Dkt. Peter Kisenge amebainisha kuwa mojawapo ya mambo wanayoyaona sasa ni kuongezeka kwa Wafanyakazi walioajiriwa ambao kazi zao zinahitaji kufikia kiwango fulani cha mafanikio (Key Perfomance Indicator-KPI's) ambao wanapata Madhara makubwa yatokanayo na Magonjwa yasiyo ya kuambukiza, hasa Presha.

Miongoni mwa Kinachosababisha changamoto hii ni Wafanyakazi hawa kuishi maisha yenye Stress pamoja na kukosa muda mzuri wa kupumzika ili watekeleze malengo waliyowekewa na taasisi zao.

Unapokwenda kununua supu, mihogo ya moto, maharage yaliyo chemshwa mtaani, ni kawaida kuona muuzaji akikufungia kwenye m...
03/06/2026

Unapokwenda kununua supu, mihogo ya moto, maharage yaliyo chemshwa mtaani, ni kawaida kuona muuzaji akikufungia kwenye mfuko wa Nailoni. Lakini, tabia hii ni salama kwa afya?

Joto kali la chakula au kinywaji linapokutana na Nailoni husababisha kemikali zenye sumu zinazoitwa Phthalates na Bisphenol A (BPA) kuyeyuka na kuingia moja kwa moja kwenye chakula chako.

Kemikali hizi zikijaa mwilini huchochea mabadiliko ya homoni, matatizo ya uzazi na hata kuongeza hatari ya Saratani. Ni salama zaidi kubeba vyombo vyako vya chuma au Udongo kutoka nyumbani unapoenda kununua vyakula vya moto.

02/06/2026

Bingwa wa Uzazi na Magonjwa ya Wanawake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Nathanael Mtinangi anashauri wanandoa wanaohangaika kutafuta Watoto wasishiriki tendo la ndoa kila siku ili kumpa nafasi Mwanaume kutengeneza mbegu nyingi, zenye Ubora unaoweza kurutubisha yai.

Katika mahojiano haya yaliyofanyika kupitia Mwananchi Digital, Dkt. Mtinangi anabainisha kuwa njia hii inaweza kuongeza uwezekano kwa Mwanamke kupata Ujauzito hasa ikiwa changamoto inatoka kwa Mwanaume

01/06/2026

Haya yamesemwa na Asha Omar Rashid, Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), alipokuwa akichangia Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Juni 1, 2026

Ameiomba Serikali kuweka Sheria kali na kupiga Marufuku midoli kuvalishwa nguo za ndani kwani inadhalilisha Wanawake.

Nini maoni yako?

01/06/2026

Kila anapojisafisha na vibomba vya bafuni, mwanamke anajiongezea hatari ya maambukizi ukeni kwani hutoa maji kwa kasi kubwa inayovuruga uwiano wa Bakteria wazuru wanaopatikana sehemu hiyo

Ufafanuzi huu umetolewa na Dkt. Sadru Mohamed,
Mwanzilishi wa App ya AfyaChap na Mmiliki wa Kliniki ya Madaktari Bingwa ya Royal iliyopo Musoma-Mara, Tanzania kupitia ST BONGO TV

01/06/2026

Mbunge wa Kigoma Mjini (CCM), Clayton Revocatus Chipando, anayejulikana zaidi kwa jina lake la kimuziki, Baba Levo, amesema haya Juni 1, 2026, akichangia Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Bungeni, Dodoma

Nini maoni yako?

Mara ya mwisho kutembea juu ya nyasi au mchanga bila viatu ilikuwa lini? Siku hizi wengi wetu tunavaa viatu muda wote, h...
01/06/2026

Mara ya mwisho kutembea juu ya nyasi au mchanga bila viatu ilikuwa lini? Siku hizi wengi wetu tunavaa viatu muda wote, hivyo tunakosa muda wa kuwasiliana moja kwa moja na Mazingira ya asili.

Wataalamu wengine huiita hali hii “Grounding” au “Earthing.” Ingawa bado hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha madai yote ya kiafya yanayoenezwa jambo hili, Watu wengi huripoti kujisikia vizuri zaidi, kupata utulivu wa akili na wakati mwingine Usingizi bora baada ya kutumia muda kwenye Mazingira ya asili.

Jaribu kutenga dakika 15 hadi 30 kila siku kutembea juu ya nyasi au mchanga ukiwa bila viatu, hasa sehemu salama na safi. Ni njia rahisi ya Kupumzika, kupata hewa safi na kuupa Mwili na akili muda wa kutulia bila gharama yoyote

31/05/2026

Mazoea ya kunywa P2 k**a karanga huharibu Mzunguko wa Hedhi na kusababisha changamoto za uzazi

Dkt. Sadru Mohamed,
Mwanzilishi wa App ya AfyaChap na Mmiliki wa Kliniki ya Madaktari Bingwa ya Royal iliyopo Musoma-Mara, Tanzania.

Credit: ST BONGO TV

Mtindi unaweza kusaidia kuondoa changamoto ya Choo Kigumu kwakuwa ni chanzo kizuri cha Probiotics (Bakteria wazuri) amba...
30/05/2026

Mtindi unaweza kusaidia kuondoa changamoto ya Choo Kigumu kwakuwa ni chanzo kizuri cha Probiotics (Bakteria wazuri) ambazo husaidia kuleta usawa wa Bakteria kwenye Tumbo, hivyo kuboresha mmeng'enyo wa chakula.

Pia, huwa na Asidi ya Laktiki (Lactic Acid) inayoweza kusaidia katika kuongeza mijongeo ya Tumbo na Utumbo hivyo kupunguza ugumu wa Choo.

30/05/2026

Alberto Mwapinga ni Daktari wa Magonjwa ya Afya ya Akili pamoja na Ushauri wa Saikolojia kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa kitengo cha afya ya Akili, amesema yapo malezi ambayo yanaweza kusababisha changamoto ya afya ya akili kwa mtoto k**a mzazi kuwa na msimamo mkali kwa mtoto na kuturuhusu Watoto kuhoji.

Dkt. Mwapinga anabainisha malezi hayo ya aliyoyaita 'Msimamo mkali' husababisha Changamoto za afya ya akili kwa mtoto k**a Sonona na wasiwasi uliopitiliza

Video: Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share