23/04/2026
UGONJWA WA FIGO KUFELI AU KUSHINDWA KUFANYA KAZI(KIDNEY FAILURE),CHANZO,DALILI,NA MATIBABU
0716 535 237
Ugonjwa wa kufeli kwa figo ni ugonjwa ambao huwapata watu wengi na sababu kubwa zikitokana na mtindo mbaya wa maisha ikiwemo ulaji mbaya,matumizi ya pombe kupita kiasi,Uvutaji wa Sigara, tatizo la kuwa na uzito mkubwa kupita kiasi,matumizi ya baadhi ya dawa,kutokufanya mazoezi n.k
KUFELI KWA FIGO KUNAWEZA KULETA MATATIZO mbali MBALI MWILINI K**A
1-Uvimbe wa Miguu n.k
2- viwango vya asidi kuongezeka,
3-viwango vya potasiamu kuongezeka
4-viwango vya kalsiamu kuongezeka
5-viwango vya phosphate kuongezeka
AINA MBILI KUU ZA KUFELI KWA FIGO
(i) Figo kushindwa kufanya kazi ndani ya mda mfupi kwa kitaalam tunaita Acute kidney Failure,
(ii) Figo kushindwa kufanya kazi au kuwa na ugonjwa sugu wa figo ambapo kitaalam hujulikana k**a Chronic kidney failure ambao mara nyingi hauwezi kutibika kabsa.
SABABU ZA FIGO KUFELI
1.Kisukari ni miongoni mwa sababu kubwa zinazochangia kutokea kwa ugonjwa wa kufeli kwa figo,
3.Ugonjwa wa Presha au Shinikizo la damu usipodhibitiwa vizuri,huweza kuwa chanzo kikubwa cha ugonjwa wa kufeli kwa figo au figo kushindwa kufanya kazi,
4. uvimbe kwenye figo zote mbili na mara nyingi ugonjwa huu unaweza kurithiwa kutoka kwa wazazi.
5. Sababu zingine za kutokea kwa Ugonjwa wa kufeli kwa figo ni pamoja na;
6.Umri mkubwa wa figo au Figo kuzeeka
7.Tatizo la kufunga kwa mishipa iendayo kwenye figo
8.Uwepo wa mawe ya Figo(Kidney Stones)
9.Tatizo la figo kushambuliwa na magonjwa ya mara kwa mara
DALILI ZA UGONJWA WA KUFELI KWA FIGO-KIDNEY FAILURE
(1) Tatizo la Kuvimba uso,Miguu na tumbo
Japo si kila uvimbe hutokana na tatizo la kufeli kwa Figo(kidney failure).
(2) Tatizo la Kukosa hamu ya chakula, kichefuchefu, na kutapika
(3) Kupata tatizo la presha au Shinikizo la damu
(4)Tatizo la ukosefu wa damu
(5) Tatizo la kupata maumivu ya mgongo,kujikuna na maumivu ya miguu (cramps) pamoja na Maumivu wakati wa kukojoa
DALILI ZINGINE ZINAZOHUSU MKOJO NI PAMOJA NA
1. Kiwango cha Mkojo kupungua
2. Kupata Muwasho wakati wa kukojoa
3. kukojoa mara kwa mara
4. kukojoa damu au usaha
5. Ugumu wa kukojoa
KWA USHAURI ZAIDI/ELIMU/TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255794897240
Dar es salaam