Afya ya mama na mtoto

Afya ya mama na mtoto Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Afya ya mama na mtoto, Health & Wellness Website, Dar es Salaam.

Paul Damas is medical personal who qualified to practice, care ,and support patient with different conditions, providing health education as long as advice to ensure health to the whole community

Hello friends nice things are coming please be humble
09/01/2026

Hello friends nice things are coming please be humble

14/05/2025

Je unafahamu umuhimu wa kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi pale tuu unapoonza clinic?
Je ulishajiuliza kwa nini mama anapimwa vipimo vingi kuliko Baba ?
Mama anapoanza clinic huwa anapimwa vipimo vingi k**a vile homa ya ini (hepatitis B),malaria(MRDT) ,Mkojo (urinalysis),sukari,(RBG) grupu la damu blood grouping, wingi wa damu haemoglobin level (Hb),picha ya kizazi obstetrics utlasound hapa kila kipimo kina maana kubwa Sana lakin turudi kweli mada au maswali yetu ntakuja na maelezo ya kila kipimo kwa leo nitazungumzia kwa nini mama atumie duo yaan kipimo cha magonjwa mawili ya zinaa k**a kaswende na maambukizi ya virusi ukimwi lakini Baba anapimwa tuu ukimwi lengo kubwa ni kibaini kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto PMTCT alieko katika kizazi uterusi kwa kipindi hiki hivyo Baba hupimwa ili aweze kubainika hali yake na pia mama hupimwa ili k**a mmoja au wote ni wanamaambukizo waweza kupewa elimu juu ya ugonjwa gani waishi katika kipindi hiki cha mimba Hadi kujifungua hivyo ni muhimu Sana kupima maambukizi ya virusi ya ukimwi iwapo watabainika kuwa na upungufu wa kings mwilini basi wataunganishwa kitengo cha matunzo na tiba kwa wagonjwa wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi lakini pia syphilis au kaswende ni ugonjwa hatari kwa mjamzito anapaswa kupata matibabu kulingana na mwingozo wa wizara ya afya ili asipate athari zitokanazo ugonjwa huo k**a vile mimba kuharibika kulika kizazi upofu kwa mtoto kufariki kwa mtoto siku chache baadae ya kujifungua
Iwapo mama atakuwa na maambukizi ataanzishiwa dawa za kufubaza maambukizi ya virusi vya ukimwi lakin pia anapimwa CD4 na anapimwa kiwango cha virusi kwenye damu HVL ili tuweze kujua hali yake k**a NI high risk au low risk mama tafatiliwa kwa karibu ili kusudi mtoto aweze kukingwa vizuri.
K**a mama atakuwa na high viral load basi mtoto atachukuliwa kipimo pale Tu anapozaliwa then 6 week then 9 month then akitimiza mwaka then baadae ya hapo ni 18-24 for confirmation lakin kwa Yule high risk atapewa dawa king atatumia Hadi afikishe miaka 2 lakin iwapo mtt anapimwa akabainika ni positive ataanzishiwa dawa za kufubaza maambukizi ya virusi vya ukimwi
K**a mama hatokuwa na maambukizi lakin Baba anayo basi Baba ataunganishwa na huduma ya matunzo na atashauriwa kutumia kondomu ili amkinge mama juu ya maambukizi lakin pia mama atapewa dawa kinga za maambukizi PREP lengo ni kumkinga na maambukizi kutoka kwa Baba dawa hizi atatumia kwa muda wote atakaoishi na mwenzio wake na mama akiwa anatumia Prep hawezi kupata maambukizi. Hadi wakati mwingine

Je unasumbua we mwanamke/mwanamke kwenye masuala ya uzazi  karibu tukuhudumie
07/05/2025

Je unasumbua we mwanamke/mwanamke kwenye masuala ya uzazi karibu tukuhudumie

MAKUNDI MATANO MUHIMU KWA MAMA MJAMZITO MTOTO ZAIDI YA MIEZI SITA AU MAMA ANAENYONYESHA NI :-1.MAKUNDI YA VYAKULAMakundi...
23/04/2025

MAKUNDI MATANO MUHIMU KWA MAMA MJAMZITO MTOTO ZAIDI YA MIEZI SITA AU MAMA ANAENYONYESHA NI :-

1.MAKUNDI YA VYAKULA
Makundi ya vyakula na mlo kamili/Mlo mchanganyiko

VYAKULA VYA PROTIN
Vyakula vyenye asili ya wanyama: Vyakula vyenye asili ya wanyama ni pamoja na nyama, samaki, dagaa, maziwa, mayai, jibini, maini, figo, senene, nzige, kumbikumbi na wadudu wengine wanaoliwa.

Husaidia mwili kukarabati sehemu zilizo chakaa, kuimarisha kinga ya mwili, kuzuia upungufu wa damu na kuuwezesha mwili kufanya kazi kwa ufanisi.

2. VYAKULA VYA WANGA

Vyakula vya nafaka, mizizi na ndizi: Vyakula hivi ndivyo vinavyochukua sehemu kubwa ya mlo na kwa kawaida ndiyo vyakula vikuu. Vyakula katika kundi hili ni pamoja na mahindi, mchele, mtama, ulezi, ngano, uwele, viazi vikuu, viazi vitamu, muhogo, magimbi, viazi mviringo na ndizi.
Huupa mwili nguvu ya kufanya kazi

3. VYAKULA VYA VITAMIN NA MADINI

Matunda: Kundi hili linajumuisha matunda ya aina zote k**a papai, embe, pera, limau, pesheni, nanasi, peasi, chungwa, chenza, zambarau, parachichi, ndizi mbivu, fenesi, stafeli, mabungo, madalansi, pichesi na topetope. Aidha ikumbukwe kuwa matunda pori au yale ya asili yana ubora sawa na matunda mengine. Matunda hayo ni k**a ubuyu, ukwaju, embe ng’ongo, mavilu na mikoche. Sungwi

Huupa mwili uwezo wa kuzuia na kupambana na maradhi na kuwezesha mwili kufanya kazi kwa ufanisi. Pia husaidia kulainisha choo

4. MBOGA MBOGA
Kundi hili linajumuisha aina zote za mboga-mboga zinazolimwa na zinazoota zenyewe. Mboga-mboga ni pamoja na mchicha, majani ya maboga, kisamvu, majani ya kunde, matembele, spinachi, mnafu, mchunga. Aina nyingine za mboga-mboga ni pamoja na karoti, pilipili hoho, biringanya, matango, maboga, nyanya chungu, bamia, bitiruti, kabichi na figiri.

Huupa mwili uwezo wa kuzuia na kupambana na maradhi na kuwezesha mwili kufanya kazi kwa ufanisi. Pia husaidia kulainisha choo

5. VYAKULA VYA MAFUTA

Mafuta: Mafuta ni muhimu lakini yanahitajika kwa kiasi kidogo mwilini. Mafuta yanaweza kupatikana kutoka kwenye mimea k**a mbegu za alizeti, ufuta, pamba, korosho, karanga na mawese. Mafuta pia yanaweza kupatikana kutoka kwa wanyama, kwa mfano: siagi, samli, nyama iliyonona na baadhi ya samaki.

Huupa mwili nguvu kwa kiasi kikubwa

Maji: Inapaswa kunywa maji safi na salama ya kutosha, angalau lita moja na nusu (au glasi nane) kwa siku ili kuzuia kusaidia maziwa kuzalishwa kwa wingi. Vile vile unaweza kuongeza maji mwilini kwa kunywa vinywaji k**a supu, madafu, togwa na juisi halisi za matunda mbalimbali.

Husaidia maziwa kutoka kwa wingi na kuzia upungufu wa maji mwilini

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya ya mama na mtoto posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share