Mam afya clinic

Mam afya clinic AFYA YAKO KIPAUMBELE CHETU
KARIBU TUKUHUDUMIE
0655863543

05/04/2026
New sh 10,000
18/12/2025

New sh 10,000

Saratani ya tezi dume ni ugonjwa unaowapata wanaume, ambapo seli za tezi hiyo huanza kukua bila mpangilio na kuunda uvim...
29/07/2025

Saratani ya tezi dume ni ugonjwa unaowapata wanaume, ambapo seli za tezi hiyo huanza kukua bila mpangilio na kuunda uvimbe. Ingawa chanzo halisi hakijulikani kikamilifu, kuna mambo kadhaa yanayochangia kuongezeka kwa hatari ya kupata ugonjwa huu:

Sababu Zinazochangia Saratani ya Tezi Dume

1. Umri mkubwa: Hatari huongezeka kwa wanaume wanapozeeka, hasa kuanzia miaka 50 na kuendelea.

2. Historia ya familia: Kuwa na ndugu wa karibu (k**a baba au kaka) aliyewahi kuugua saratani ya tezi dume huongeza uwezekano wa kupata ugonjwa huu.

3. Asili ya kiafrika: Wanaume wenye asili ya Kiafrika wana hatari kubwa zaidi ya kupata saratani ya tezi dume ikilinganishwa na makabila mengine.

4. Lishe isiyofaa: Ulaji wa nyama nyekundu na iliyosindikwa, bidhaa zenye mafuta mengi, na vyakula vyenye sukari nyingi unaweza kuongeza hatari ya saratani hii.

5. Unene kupita kiasi (obesity): Uzito mkubwa umehusishwa na hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume.

6. Mabadiliko ya vinasaba (DNA mutations): Mabadiliko katika vinasaba, hasa BRCA1 na BRCA2, yanaweza kuongeza hatari ya saratani ya tezi dume.

7. Maambukizi na uvimbe wa tezi dume (prostatitis): Maambukizi ya mara kwa mara au uvimbe wa tezi dume unaweza kuchangia hatari ya saratani.

Tahadhari na Uchunguzi

Kwa kuwa saratani ya tezi dume mara nyingi haina dalili za mapema, ni muhimu kwa wanaume hasa walio na umri wa miaka 50 na kuendelea, au wale walio katika makundi ya hatari, kufanya uchunguzi wa mara kwa mara k**a vile kipimo cha PSA (Prostate-Specific Antigen) na uchunguzi wa daktari.

Kufanya maamuzi ya kiafya yanayolenga mtindo wa maisha bora, k**a vile kula lishe yenye matunda na mboga, kufanya mazoezi ya mara kwa mara, na kuepuka vyakula vyenye mafuta mengi, kunaweza kusaidia kupunguza hatari ya kupata saratani ya tezi dume.

Kwa habari zaidi na msaada wa kitaalamu, unaweza kutembelea Ocean Road Cancer Institute au vituo vingine vya afya vilivyo karibu nawe.

Je unasumbuliwa na uzimbe karibu tukusaidie 0655863543
14/07/2025

Je unasumbuliwa na uzimbe karibu tukusaidie 0655863543

0655863543
13/07/2025

0655863543

12/07/2025

MUHTASARI KUHUSU TEZI DUME

🔵 Tezi Dume ni nini?
Tezi dume ni kiungo kidogo cha mfumo wa uzazi wa mwanaume, kilicho chini ya kibofu cha mkojo, na huzalisha majimaji ya mbegu yanayosaidia kurutubisha yai la mwanamke.

🔵 Mabadiliko ya Tezi Dume
Kadri mwanaume anavyozeeka, tezi dume inaweza kuongezeka ukubwa (BPH), na kusababisha matatizo ya njia ya mkojo k**a:

Kukojoa mara kwa mara, hasa usiku

Kukojoa kwa shida au mkojo kudondoka

Maumivu wakati wa kukojoa

🔵 Saratani ya Tezi Dume
Ni aina ya saratani inayowapata wanaume. Huwa kimya mwanzoni bila dalili, lakini inaweza kugundulika kwa uchunguzi wa mapema. Dalili hujumuisha:

Maumivu ya nyonga au mgongo

Mkojo kuwa na damu

Kupungua kwa nguvu za kiume

🔵 Namna ya Kujikinga au Kugundua Mapema
✅ Fanya uchunguzi wa afya mara kwa mara (PSA test au DRE)
✅ Kula lishe bora (matunda, mboga, epuka vyakula vya mafuta sana)
✅ Fanya mazoezi
✅ Epuka kuvuta sigara na kunywa pombe kupita kiasi

🔵 Ujumbe Muhimu
Tezi dume siyo aibu! Elimu na uchunguzi wa mapema vinaweza kuokoa maisha.
👉 Tafadhali shiriki ujumbe huu kuelimisha wengine.

11/07/2025

*Kisukari ni Nini?*

*Kisukari ni ugonjwa wa kimetaboliki ambao* *husababisha viwango vya sukari katika damu kuwa juu zaidi ya* *kiwango cha kawaida.*

Huu ugonjwa unapotokea, mwili hauwezi kutumia sukari (glucose) kwa ufanisi, ambayo inaweza kuathiri jinsi unavyojisikia na hata kupelekea matatizo mengine ya kiafya.

Dhibiti Kisukari
Kwa mara ya kwanza tunakusaidia kudhibiti kisukari kupitia ushauri wetu wa kitaalamu usiojali umbali uliopo kati yako na daktari

Fahamu zaidi
Kisukari ni Ugonjwa Gani?
Kisukari, au ugonjwa wa kisukari, ni ugonjwa sugu ambapo mwili hawezi kudhibiti viwango vya sukari kwenye damu.

Mwili hushidnwa kudhibiti sukari kwasababu ya matatizo katika utendaji wa insulini, homoni inayosaidia kuingiza sukari kwenye seli za mwili kutumika k**a nishati au kuihifadhi.

Ingawa wengi hufahamu aina mbili za kisukari, ukweli ni kwamba aina za kisukari sipo Aina mbili nakuendelea

Aina za Kisukari
Kisukari Aina ya Kwanza (Type 1 Diabetes): Hii ni aina ya kisukari ambapo mwili hauwezi kutoa insulini kutokana na uharibifu wa seli za kongosho. Kisukari aina ya kwanza mara nyingi hutokea kwa watu wenye umri mdogo.

Kisukari Aina ya Pili (Type 2 Diabetes): Aina hii hutokea wakati mwili hawezi kutumia insulini ipasavyo au hutoa insulini kwa kiasi kidogo. Kisukari aina ya pili mara nyingi huathiri watu wazima na inahusishwa na uzito kupita kiasi na mtindo wa maisha usio bora.

Kisukari cha Mimba (Gestational Diabetes): Hutokea wakati wa ujauzito na huweza kupona baada ya kujifungua. lakini wanawake wenye kisukari cha mimba wana hatari kubwa ya kupata kisukari aina ya pili baadaye maishani.

Kisukari kinachotokana na magonjwa mengine, mfano ugonjwa wa matezi kwenye figo na kwenye mayai ya uzazi ya mwanamke. Magonjwa haya husababisha kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu. Lakini yanatibika na hivyo aina hii ya kisukari hutibika.
Madhara ya Ugonjwa wa Kisukari
Kisukari kinapototolewa bila udhibiti, kinaweza kusababisha madhara mbalimbali k**a vile matatizo ya moyo, kushuka kwa kiwango cha kuona, magonjwa ya figo, na matatizo ya vidole k**a vile vidonda vinavyochelewa kupona.

Pia, inaweza kusababisha uharibifu wa mishipa ya damu na neva
*Tibu sukari Leo kwa gharama ndogo ya ofa Leo* *+255655863443

Unataka kujisafisha mwili wako na kuimarisha afya ya uzazi? Hii ndio suluhisho lako!Yoni Pearls ni tiba ya asili inayosa...
16/09/2024

Unataka kujisafisha mwili wako na kuimarisha afya ya uzazi?

Hii ndio suluhisho lako!

Yoni Pearls ni tiba ya asili inayosaidia kusafisha uke, kuondoa sumu, na kurejesha usawa wa mwili wa mwanamke.

Imetengenezwa kwa mimea asilia na imekuwa ikitumika kwa miaka mingi kuboresha afya ya uzazi.

Jisikie safi na huru! Kwa kutumia Yoni Pearls, utaondokana na harufu mbaya, maambukizi, cyst, na matatizo ya uzazi huku ukiimarisha afya ya uke na kuboresha mzunguko wako wa hedhi.

Usikose fursa hii! Jipatie Yoni Pearls yako sasa kwa bei ya punguzo kwa sh 15,000 badala ya sh 30,000
okoa sh 15,000

Piga simu 0655-863543 na uagize leo!

Address

Muheza Tanga
Tanga

Telephone

+255655863543

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mam afya clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share