21/07/2021
Siri kuu 4 za unga wa mbegu za maboga.
1. Husaidia kuondoa tatizo la kukosa usingizi kwa kuwa ina "Tryptophan" kwa wingi ambayo husaidia kuleta usingizi.
2. Una kambakamba (fibre) ambazo husaidia mmeng'enyo wa chakula na kurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu.
3. Husaidia afya ya moyo kwa kuwa na kiwango kikubwa cha madini ya Magnesium.
4. Una viondoa sumu mwilini (antioxidants) ambavyo huukinga mwili wako na msongo wa sumu na magonjwa.