04/03/2026
🌿 Bawasiri (Hemorrhoids) ni uvimbe wa mishipa ya damu kwenye njia ya haja kubwa (mkundu). Hutokea ndani au nje ya mkundu.
✅ *Sababu za kupata bawasiri*
🍡Kujikaza sana wakati wa kujisaidia (hasa ukiwa na choo kigumu).
Kufunga choo (constipation) mara kwa mara.
🍡Kukaa muda mrefu chooni au kukaa sana bila kusimama.
🍡Lishe isiyo na nyuzinyuzi (fiber) – kula vyakula visivyo na mboga na matunda.
🍡Ujauzito – presha kwenye mishipa ya damu huongezeka.
🍡Unene kupita kiasi.
Kuinua vitu vizito mara kwa mara.
⚠️ *Madhara ya bawasiri*
🍡Maumivu makali wakati wa kujisaidia.
🍡Kutoka damu wakati wa haja kubwa.
🍡Kuwashwa au kuungua mkunduni.
🍡Uvimbe au kitu kutoka nje ya mkundu.
🍡Upungufu wa damu (ikiwa damu inatoka mara kwa mara).
🍡Maambukizi k**a haitatibiwa mapema.
🌱 *Jinsi ya kujikinga (kwa ufupi)*
✅Kula vyakula vyenye nyuzinyuzi nyingi (mboga, matunda).
✅Kunywa maji mengi.
✅Epuka kujikaza chooni.
Fanya mazoezi mara kwa mara.