25/03/2023
KWA NINI VINATOKA VINYAMANYAMA AU MABONGE YA DAMU WAKATI WA HEDHI
Kwa asili, wanawake wengi huwa wanapatwa na hali hii ya mabonge wanapokuwa hedhini, ni jambo ambalo huwastusha wengi na hutufanya kuwa na maswali k**a vile â¢Kwa nini mwanamke anatokwa na damu iliyoganda wakati wa hedhi?
â¢Ni kipi hasa husababisha damu kuganda wakati wa hedhi?
Leo nipo kwa ajili ya majibu.
~~Kwa ujumla, chanzo cha kuganda kwa damu wakati wa hedhi yako hutokana na kushindwa kutoka kwa ute wenye kemikali unaozuia kuganda kwa damu kibaolojia huitwa anticoagulants......
ambapo kazi ya ute huu ni kuukinga ukuta wa kizazi usiharibike.
Wakati wa hedhi, ute mzito unakuwa kwenye ukuta wa kizazi huanza kutoka. Ute huu unaokuwa na kemikali huanza kuachiliwa ili kuzuia damu isigande wakati wa hedhi. Wanawake wengi wanaotokwa na damu ya hedhi muda mrefu hutoka na damu yenye mabonge kwa sababu damu inayotoka kwenye ukuta wa mfuko wa kizazi(uterus) hutoka kwa kasi kuliko ute wenye kemikali ya kuiyeyusha isigande. Hali hii ndio husababisha damu kuganda na hedhi kutoka na mabonge ya damu kwa muda mrefu.
Visabibishi vya kupungua kwa ute huu (anticoagulants) ni uwepo wa tatizo katika kizazi mfano.
1. Uvimbe Katika Kizazi (Uterine Fibroids)
Uvimbe mmoja au zaidi ambao huwa sio saratani, kwa kawaida huota ndani ya kizazi cha mwanamke. Hata hivyo kwa kuwa sio saratani, huwa havionyeshi kuwa vimetulia tu. Dalili za kawaida anazozipata mwanamke mwenye uvimbe aina ya fibroids ni k**a ifuatavyo:
â¢Maumivu ya tumbo chini ya kitovu
â¢Maumivu wakati wa tendo la ndoa
â¢Kutokwa na damu ya hedhi muda mrefu
â¢Tumbo kujaa gesi ama kukosa choo
2. Matumizi ya njia za Kisasa za Uzazi Wa Mpango
Dhumuni kuu la njia za kisasa za Uzazi wa mpango ni kuvuruga mpangilio wa homoni za mwanamke. Kivurugika kwa homoni hauharibu tu ukomavu wa mayai bali huharibu vichochezi vya homoni hasa oestrogens na progesterone ambazo ni muhimu katika kuzalisha ute, mayai na ujauzito kwa ujumla.
JICHUNGUZE
Ikiwa k**a unapaswa kubadilisha pedi zaidi ya mara moja kila baada ya masaa mawili au k**a mtiririko wa damu yako ya hedhi una mabonge makubwa ya damu yasiyokuwa ya kawaida, basi ina maanisha kwamba unatokwa na damu nyingi mno.
Endapo k**a utagundua kuwa mtiririko huo wa damu ulianza tu kipindi ulipoanza kutumia aina mpya ya vidonge vya mpango wa uzazi, basi unapaswa umweleze daktari wako akupe usahuri kuhusu jambo hilo.
3. Kuporomoka Kwa Mimba
5. Maambukizi
Aina ya kwanza ya maambukizi yanayoweza kusababisha hali hii ya kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi ni maambukizi katika via vya uzazi(P.I.D). Maambukizi ya aina hii huathiri viungo vya uzazi kwa mwanamke, na k**a tatizo hili litaendelea bila kufahamika vizuri, basi linaweza kusababisha uharibifu mkubwa katika mfumo wa uzazi wa mwanamke.
Uonapo dalili za kuwa mabonge wakati wa hedhi unaweza kumuona daktari wako kwa vipimo zaidi ila k**a umegundua tayari una mojawapo ya magonjwa hapo juu au umewahi kutumia uzazi wa mpango, jitahidi kutumia vyakula au vinywaji vyenye kukusaidia kuweka homoni sawa na kuyeyusha damu ili isikwame katika mfumo wa uzazi.
Muhimu k**a umegundua una matatizo katika uzazi ni vyema kuanza dozi yako ya kusafisha NJIA za Uzazi na kuweka homoni sawa ili uendelee kuwa na mrejesho mzuri siku zote.
Yapo mengi ya kuzungumza kuhusu uzazi hatuwezi kumaliza leo, endelea kufuatilia mafundisho haya pia unaweza kuwasiliana nami kwa mazungumzo zaidi....
0621672394