04/03/2023
JE?WAJUA KUWA MSH*TUKO WA MOYO (HEART ATTACK) UNATIBIKA
Msh*tuko wa moyo hutokea pale mtiririko wa damu kuelekea kwenye moyo unapozibwa. Mara nyingi kuziba huku hutokana na kujikusanya kwa mafuta, cholesterol na vitu vingine, ambavyo hufanya utando ndani ya ateri zinazopeleka damu kwenye moyo (coronary arteries). Mara nyingine utando huu hubomoka na kufanya donge la damu linaloziba mtiririko wa damu. Kuziba huku kwa damu kunaweza kuharibu sehemu ya musuli wa moyo.
Mshtuko wa moyo, ambao kitaalamu huitwa myocardial infarction, unaweza kuua, lakini siku za karibuni tiba yake imeboreshwa. Ni muhimu kupiga 911 au namba ya dharula endapo unahisi unanyemelewa na mshtuko wa moyo.
Dalili Za Msh*tuko Wa MOYO
Dalili za kawaida za msh*tuko wa moyo ni pamoja na: Pressure, kubana kifua, maumivu, na kubana au kuwashwa kifuani na mikononi kunakoweza kuenea hadi maeneo ya shingo, taya au mgongoni Kichefu, kuvimbiwa, kiungulia au maumivu ya tumbo Kuhema kwa shida Jasho baridi Uchovu Kizunguzungu cha ghafla
Dalili Za Msh*tuko Wa Moyo Hutofautiana
Si watu wote wanaopata msh*tuko wanapata dalili zile zile au za uzito ule ule. Wengi hupata maumivu ya kiasi, wengine maumivu makali. Wengine hawaoni dalili zo zote. Kwa baadhi yao, dalili ya kwanza ni moyo kusimama kufanya kazi.
Mash*tuko wa moyo mara nyingine huja ghafla, lakini kwa watu walio wengi, dalili huonekana saa, siku au hata wiki kadhaa kabla. Dalili ya wawali kabisa yaweza kuwa maumivu kifuani yanayojirudia (angina) yanayoanza unapokuwa na shughuli na kuacha ukipumzika. Angina husababishwa na kupungua kwa muda mfupi kwa mtiririko wa damu kwenye moyo.
Nini Cha Kufanya K**a Unaona Mtu Amepatwa na Msh*tuko Wa Moyo
K**a unamwona mtu amepoteza fahamu na unahisi amepata msh*tuko wa moyo, kwanza piga simu kuomba msaada wa dharula. Kisha chunguza k**a anapumua na ana mapigo ya moyo. K**a hapumui na hana mapigo ya moyo, mpe huduma ya CPR.
Sukuma kwa nguvu na kwa haraka juu ya kifua chake ukitumia misukumo ya haraka inayolingana – k**a misukumo 100 hadi 120 kwa dakika.
Chanzo Cha Msh*tuko Wa Moyo
Msh*tuko wa moyo unatokea wakati ateri moja au zaidi ya moja ya kupeleka damu kwenye moyo inapoziba. Muda ukienda, mafuta ikiwa ni pamoja na cholesterol, hujijenga na kutengeneza plaque, ambayo itapunguza kipenyo cha ateri (atherosclerosis). Hali hii, iitwayo ugonjwa wa ateri za moyo (coronary artery disease), ndicho chanzo cha mish*tuko ya moyo iliyo mingi.
Wakati msh*tuko unapotokea, plaque inaweza kuwa imebomoka na kumwaga cholesterol na vitu vingine ndani ya mkondo wa damu. Donge la damu hutokea eneo plaque ilipobomoka. Endapo donge hilo ni kubwa, linaweza kuziba mtiririko wa damu ndani ya ateri, na kuufanya moyo ukose oksijeni na virutubishi (ischemia).
Unaweza kuwa na tatizo la mishipa kuziba kiasi au kuziba kabisa.
Ikiziba kabisa una ST elevation myocardial infarction (STEMI). Ikiziba kiasi una non-ST elevation myocardial infarction (NSTEMI).
Uchunguzi na tiba hutofautiana kulingana na aina ya tatizo ulilo nalo.
Sababu nyingine ya msh*tuko wa moyo ni kukaza kwa ghafla kwa mshipa wa damu unaoelekea kwenye moyo (spasm of a coronary artery) ambako kutazuia damu isifike kwenye eneo fulani la musuli wa moyo. Matumizi ya tumbako na madawa ya kulevya, k**a co***ne, huweza kusababisha hali hii inayotishia maisha.
WASILIANA NASI KWA TIBA NA USHAURI
0652 400 350