Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

13/05/2026

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana yapongezwa kwa utunzaji bora wa takwimu za wagonjwa pamoja na namna wanavyo pambana katika kudhibiti na kuzuia magonjwa ya kuambukiza.


DKT. KIWELU AKIWASILI BUNGENI KUFATILIA WASILISHO LA BAJETI YA WIZARA YA AFYA KWA MWAKA WA FEDHA 2026/27Mganga Mfawidhi ...
11/05/2026

DKT. KIWELU AKIWASILI BUNGENI KUFATILIA WASILISHO LA BAJETI YA WIZARA YA AFYA KWA MWAKA WA FEDHA 2026/27

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu na baadhi ya viongozi wengine wakiwasili bungeni Jijini Dodoma kwa ajili ya kushiriki shughuli muhimu ya uwasilishaji bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 itakayowasilishwa na Waziri wa Afya Mhe.Mohamed Mchengerwa.

VIPAUMBELE 11 KUIBEBA WIZARA AFYA BAJETI, 2026/27Na Atley Kuni, WAF-DodomaWaziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesem...
11/05/2026

VIPAUMBELE 11 KUIBEBA WIZARA AFYA BAJETI, 2026/27

Na Atley Kuni, WAF-Dodoma

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Serikali imejipanga kuendelea kuboresha Sekta ya Afya nchini kupitia utekelezaji wa vipaumbele mbalimbali vitakavyoongeza upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi mijini na vijijini.

Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Mapitio ya Bajeti ya mwaka 2025/26 na Makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Mhe. Mchengerwa amesema Serikali imeelekeza nguvu katika kuboresha huduma za afya, ikiwepo bima ya afya kwa wote, kuongeza wataalam pamoja na kuimarisha matumizi ya teknolojia katika hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya.

"Serikali itaendelea kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zenye staha na utu kwa kuboresha mazingira ya utoaji huduma, kupunguza muda wa kusubiri matibabu na kuimarisha mifumo ya kushughulikia malalamiko ya wananchi katika vituo vya afya", amesema Mhe.Mchengerwa.

Katika kuwapunguzia wananchi mzigo wa gharama za matibabu, Waziri Mchengerwa amesema Serikali itaendelea na utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kusajili kaya zenye uhitaji pamoja na kuhamasisha wananchi wengi zaidi kujiunga na huduma hiyo muhimu.

Aidha, Serikali imepanga kuongeza uwekezaji katika viwanda vya ndani vya dawa na bidhaa za afya ili kuhakikisha upatikanaji wa dawa muhimu unaimarika na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje ya nchi.

Waziri Mchengerwa amefafanua kuwa Serikali inatarajiwa kuongeza ajira na kukuza uchumi wa ndani, sambamba na kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika Sekta ya Afya kwa kuunganisha mifumo ya taarifa za afya, kuongeza huduma za afya mtandao pamoja na matumizi ya akili unde kwenye kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika upande wa huduma za kinga, Mchengerwa amesema, Serikali imeweka mkazo kwenye mapambano dhidi ya magonjwa ya mlipuko, magonjwa yasiyoambukiza pamoja na kuendelea kuimarisha huduma za chanjo nchini.

"Katika Mwaka ujao wa fedha wahudumu wa afya ngazi ya jamii 8,000 wanatarajiwa kuajiriwa ili kuongeza huduma za afya kwa wananchi maeneo mbalimbali nchini.

*SERIKALI YATOA BILIONI 48.8 BIMA YA AFYA KWA WOTE**• Wanufaika 463,228 waanza kupata huduma za matibabu*Serikali imeanz...
11/05/2026

*SERIKALI YATOA BILIONI 48.8 BIMA YA AFYA KWA WOTE*

*• Wanufaika 463,228 waanza kupata huduma za matibabu*

Serikali imeanza rasmi utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kaya zisizo na uwezo, baada ya kutoa Shilingi bilioni 48.8 kwa ajili ya kuwawezesha wananchi wa makundi maalum kupata huduma za afya kwa uhakika.

Kupitia utekelezaji huo, jumla ya kaya 172,297 tayari zimefikiwa na kuingizwa kwenye mpango huo, huku wanufaika 463,228 wakianza kupata huduma mbalimbali za matibabu katika vituo vilivyosajiliwa nchini.

Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya mwaka 2026/2027 Waziri wa Afya Mhe. Omary Mchengerwa alisema kuwa utekelezaji huu unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila kujali hali yake ya kiuchumi, ikiwa ni sehemu ya safari ya kuelekea huduma jumuishi za afya kwa wananchi wote.

Katika kuimarisha sekta ya afya sambamba na utekelezaji wa mpango huo, mabaraza na bodi za kitaaluma yameendelea kusimamia ubora wa huduma kwa kusajili wataalam wa afya 14,310, hatua inayoongeza nguvu kazi muhimu katika utoaji wa huduma nchini.

Alisema kuwa katika kurahisisha upatikanaji wa huduma za matibabu, jumla ya maduka ya dawa 330 yamesajiliwa pamoja na watarajali 3,004, huku vituo vya kutolea huduma za afya 3,643 vikisajiliwa ili kuongeza upatikanaji wa huduma karibu na wananchi.

Katika kuhakikisha taaluma na maadili yanaendelea kuzingatiwa hususan wakati huu wa kuhudumia wananchi wengi zaidi kupitia mfumo wa Bima ya Afya, vituo binafsi vya afya 654 vimekaguliwa ili kuhakikisha vinakidhi viwango na kutoa huduma salama kwa wananchi.

Mafanikio hayo yanaakisi hatua kubwa ya Serikali katika kujenga mfumo imara wa afya unaojali usawa, ubora na upatikanaji wa huduma kwa wote, huku Bima ya Afya kwa Wote ikiendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

WIZARA YA AFYA YAOMBA  KUIDHINISHIWA BAJETI  TRIL. 1.8 MWAKA 2026/27, FUNGU 52Na Zakayo Mosha WAF-DodomaWaziri wa Afya M...
11/05/2026

WIZARA YA AFYA YAOMBA KUIDHINISHIWA BAJETI TRIL. 1.8 MWAKA 2026/27, FUNGU 52

Na Zakayo Mosha WAF-Dodoma

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa , ameliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuidhinisha kiasi cha Shilingi trilioni 1.8 kwa ajili ya Matumizi ya Wizara hiyo katika mwaka wa fedha 2026/27 Fungu 52.

Mheshimiwa Mchengerwa ameyasema hayo leo Mei 11, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Amesema kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi Trilioni 1.148 ambazo ni sawa na asilimia 64 ya bajeti iliyotengwa zinaombwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, amesema kuwa kati fedha hizo, fedha za ndani ya nchi ni shililingi Bilioni 789.45 na kiasi cha shilingi Bilioni 358.56 zinatoka kwa washirika wa maendeleo.

Mhe.Mchengerwa ameliambia Bunge kuwa, Wizara ya Afya imepanga kutumia kiasi cha shilingi Bilioni 652.236 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambayo ni sawa na asilimia 36 ya bajeti iliyotengwa. Amefafanua kuwa kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi Bilioni 516, 323 ni kwa ajili ya mishahara ya Watumishi wa Afya na kiasi cha shilingi Bilioni 135, 913 zitatumika kwa ajili ya matumizi mengineyo

“Namshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali Watanzania na kuiwezesha Wizara ya Afya kupatiwa fedha nyingi katika miaka mitano iliyopita ambapo Nchi yetu imeendelea kuwa miongoni mwa nchi chache afrika zinazotoa matibabu kwa gharama nafu”amesema Mchengerwa.

Mwisho, Mhe. Mohamed Mchengerwa Waziri wa Afya ameliomba Bunge kuidhinisha kiasi cha jumla ya shilingi Trilioni 1.8 katika mwaka wa fedha 2026/27,amesema kupatika kwa bajeti hiyo kutasaidia kutekeleza shughuli mbalimbali zilizopangwa ikiwemo vipaumbele vyote 11 ambavyo vimelenga kuiweka Tanzania kuwa mfano kwa utoaji bora wa huduma za afya kwa Wananchi Barani Afrika

SERIKALI YAENDELEA KUPAMBANA NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZANa Hassan Kimweri, WAF - Dodoma Serikali kupitia Wizara ya Afya i...
11/05/2026

SERIKALI YAENDELEA KUPAMBANA NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

Na Hassan Kimweri, WAF - Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Afya inaendelea kuimarisha mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza nchini kwa kuongeza huduma za matibabu, vifaa tiba pamoja na upanuzi wa huduma maalum katika hospitali mbalimbali nchini.

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema hayo leo Mei 11, 2026 wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Spika wa Bunge Mhe. M***a Azan Zungu.

"Mzigo wa wagonjwa yasiyoambukiza umeongezeka kutoka wagonjwa milioni 6,502,913 mwaka 2024/2025 hadi kufikia wagonjwa milioni 6,874,308 Machi 2026, huku gharama za matibabu zikiongezeka kutoka Shilingi trilioni 1.3 mwaka 2023 hadi Shilingi trilioni 1.8 mwaka 2024," amesema Waziri Mchengerwa

Aidha, Waziri Mchengerwa amesema Wizara ya Afya imeanzisha kliniki 130 za kisukari na shinikizo la damu na kufanya idadi ya kliniki hizo kufikia 168 nchini kote, huduma za dialysis zimeongezeka hadi kufikia kuwa na vituo 74 vinavyohudumia wagonjwa 3,342.

“Serikali imeendelea kuboresha huduma za magonjwa yasiyoambukiza ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na maeneo yao pamoja na kupunguza gharama za matibabu,” amesema Waziri Mchengerwa

Kwa upande wa afya ya akili, amesema huduma zimewafikia wateja laki 254,932 huku vituo 16 vya waraibu vikitoa huduma kwa wateja elfu 17,807 na upatikanaji wa dawa za afya ya akili kufikia wastani wa asilimia 75.

"Huduma za sikoseli zimeongezeka ambapo watoto 17,245 wamepimwa, watoto 369 kugundulika kuwa na ugonjwa huo na 2,500 kubainika kuwa na vinasaba vya sikoseli, wagonjwa 42,564 wamehudumiwa," amesema Waziri Mchengerwa

Katika huduma za kinywa na meno, Waziri Mchengerwa amesema Serikali imeongeza viti 26 vya huduma na kufikisha jumla ya viti 900 pamoja na kuongeza mashine za mionzi, pia huduma za macho katika mikoa 15 zimewanufaisha watu 51,940.

*SERIKALI YAENDELEA NA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA AFYA**• Wananchi kunufaika Bima ya Afya kwa Wote*Na Grace Michael, Dodom...
11/05/2026

*SERIKALI YAENDELEA NA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA AFYA*

*• Wananchi kunufaika Bima ya Afya kwa Wote*

Na Grace Michael, Dodoma

Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kusaini Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote na usajili wa wanachama kuanza rasmi Januari 2026, Tanzania imeingia katika ukurasa mpya wa kihistoria unaolenga kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za afya k**a haki yake ya msingi.

Hatua hii inaelezwa kuwa ni mageuzi makubwa yanayodhihirisha dhamira ya Serikali ya kujenga Taifa lenye usawa wa kiafya, ambapo huduma za afya hazitakuwa tena suala la uwezo wa kifedha, upendeleo au bahati, bali haki ya kila Mtanzania popote alipo.

Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya mwaka 2026/2027 Waziri wa Afya Mhe. Omary Mchengerwa, amesema kuwa katika hatua ya utekelezaji, Serikali inaendelea kuboresha mifumo ya utoaji huduma za afya ili kuhakikisha wananchi wanaojiunga na mifumo ya bima wanapata huduma bora, za haraka na zenye viwango vinavyokidhi mahitaji ya sasa.

Sambamba na hilo, juhudi za kusajili wananchi wasio na uwezo kupitia mfumo wa kaya, zinaendelea hatua inayolenga kuwafikia Watanzania wa makundi maalum na kuwaondolea mzigo wa gharama za matibabu ambao kwa muda mrefu umekuwa changamoto kwa familia nyingi.
Amesema Serikali imejipanga kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu dhana ya Bima ya Afya kwa lengo la kuongeza uelewa wa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na mifumo mbalimbali ya bima iliyopo nchini.

Mkakati huo wa elimu unalenga kujenga jamii yenye uelewa mpana kwamba bima ya afya si chaguo la ziada, bali ni kinga muhimu ya kiuchumi na kijamii kwa familia na Taifa kwa ujumla.

“Bima ya Afya kwa Wote ni msingi wa Taifa imara, lenye wananchi wenye afya, nguvu kazi yenye tija na uchumi unaokua kwa usawa, inaweka msingi wa kupunguza umaskini unaotokana na gharama za matibabu, kuimarisha mshik**ano wa kijamii na kuongeza matumaini kwa wananchi kwamba maisha yao yanalindwa kupitia mfumo wa afya unaowajali wote,” alisema Mhe. Mchengerewa.

Kwa ujumla, kuanza rasmi kwa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ni ishara ya Tanzania mpya inayotafsiri afya k**a haki ya msingi ya mwananchi, na si fadhila.

11/05/2026
BIMA YA AFYA KWA WOTE KULETA MAPINDUZI SEKTA YA AFYA TANZANIANa Grace Michael, NHIF - DodomaTanzania inaendelea kuandika...
11/05/2026

BIMA YA AFYA KWA WOTE KULETA MAPINDUZI SEKTA YA AFYA TANZANIA

Na Grace Michael, NHIF - Dodoma

Tanzania inaendelea kuandika historia mpya katika sekta ya afya kupitia mageuzi makubwa yanayolenga kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora, salama na yenye usawa, huku Bima ya Afya kwa Wote ikiwa nguzo kuu ya kulinda familia dhidi ya umaskini unaotokana na gharama za matibabu.

Kupitia dira hiyo, Serikali inaweka msingi imara wa Taifa lenye afya bora kwa kusisitiza kuwa huduma za afya si gharama bali ni uwekezaji wa moja kwa moja katika ustawi wa wananchi na ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya mwaka 2026/27 Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema kuwa mageuzi hayo yanakusudia kuhakikisha wananchi wote, bila kujali kipato au eneo wanaloishi, wanapata fursa sawa ya huduma za matibabu, hatua inayolenga kupunguza mzigo wa kifedha kwa familia nyingi ambazo kwa miaka mingi zimekuwa zikikabiliwa na changamoto ya gharama kubwa za afya.

Amesema kuwa juhudi za kuimarisha uzalishaji wa dawa na bidhaa za afya hapa nchini zimeendelea kupewa kipaumbele k**a mkakati wa kujenga kujitegemea, kuongeza ajira kwa Watanzania na kuimarisha usalama wa Taifa katika sekta ya afya.

”Kwa mtazamo huu, dawa hazitazamwi tena k**a bidhaa ya kawaida, bali k**a sehemu muhimu ya tiba, kinga na ulinzi wa Taifa, hususan katika nyakati za changamoto za kiafya duniani,” amesema Mhe. Mchengerewa.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mchengerwa amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika mifumo ya TEHAMA sekta ya afya ili kuongeza ufanisi wa utoaji huduma, kupunguza urasimu, kuboresha uhifadhi wa taarifa za wagonjwa na kuharakisha maamuzi ya kitabibu.

“Mifumo hiyo ni nyenzo muhimu ya kuokoa maisha, kwa kuwa taarifa za mgonjwa si makaratasi ya kawaida bali ni msingi wa maamuzi ya haraka yanayoweza kuamua hatima ya maisha ya mtu,” amesema Mhe. Mchengerwa

Amesema kuwa vituo vya afya vinaendelea kupata ithibati ya ubora ili kujenga heshima, uwajibikaji na ushindani wa huduma za afya za Tanzania katika viwango vya kitaifa, kikanda na kimataifa.

BIMA YA AFYA KWA WOTE YAANZA KWA KISHINDO, WAZIRI MCHENGERWA ALIAMBIA BUNGENa Atley Kuni,  WAF-Dodoma Serikali imeanza r...
11/05/2026

BIMA YA AFYA KWA WOTE YAANZA KWA KISHINDO, WAZIRI MCHENGERWA ALIAMBIA BUNGE

Na Atley Kuni, WAF-Dodoma

Serikali imeanza rasmi utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ikiwa ni sehemu ya maboresho makubwa yanayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha ikiwa ni mwanzo wa mapinduzi mapya katika Sekta ya Afya nchini.

Hayo yamesemwa Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27, Mei 11, 2026, ambapo amesema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanaingia kwenye mfumo wa bima ya afya ili kupunguza gharama za matibabu na kuongeza usawa wa upatikanaji wa huduma za afya.

"Serikali itaendelea kusajili wananchi kutoka kaya zenye uhitaji pamoja na wale wenye uwezo ili kuhakikisha huduma za afya zinawafikia Watanzania wote bila ubaguzi", amesema Mchengerwa na kuongeza kuwa mpango huo pia utaenda sambamba na utoaji wa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kujiunga na bima ya afya.

Waziri Mchengerwa amefafanua kuwa, Serikali imeweka mikakati ya kuimarisha mfumo wa ugharamiaji wa huduma za afya kwa kutumia vyanzo vya ndani pamoja na kuongeza ushirikiano na sekta binafsi ili kuhakikisha mfumo wa bima unakuwa imara na endelevu kwa manufaa ya wananchi.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo amesema utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote utasaidia kupunguza mzigo wa wananchi kutumia fedha nyingi kupata matibabu, huku ukitarajiwa kuongeza upatikanaji wa huduma bora katika hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Kwa mujibu wa Waziri Mchengerwa, mafanikio ya mpango huo yatategemea ushiriki wa wananchi pamoja na taasisi mbalimbali kwenye kuunga mkono juhudi za Serikali za kujenga mfumo wa afya wenye usawa na unaomlinda kila Mtanzania dhidi ya gharama kubwa za matibabu.

Serikali inaamini kuwa kupitia utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, Tanzania itaingia katika hatua mpya ya kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwa urahisi zaidi, huku wananchi wakiondokana na hofu ya kushindwa kupata matibabu kutokana na changamoto za kifedha.

KIPINDI CHA MWAKA 2021-2026 HUDUMA ZA AFYA ZIMEONGEZEKA, ZIMEIMARIKANa Hassan Kimweri, WAF - DodomaSekta ya afya nchini ...
11/05/2026

KIPINDI CHA MWAKA 2021-2026 HUDUMA ZA AFYA ZIMEONGEZEKA, ZIMEIMARIKA

Na Hassan Kimweri, WAF - Dodoma

Sekta ya afya nchini imepata mafanikio makubwa katika kipindi cha awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yaliyoongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi kupitia ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa vifaa tiba, uoatikanaji wa dawa pamoja na huduma za kibingwa na za dharura nchini.

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema hayo leo Mei 11, 2026 wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Spika wa Bunge Mhe. M***a Azan Zungu.

"Eneo la vituo vya kutolea huduma za afya vimeongezeka kutoka elfu 10,153 mwaka 2021/22 hadi elfu 13,683 kufikia Machi 2026, sawa na ongezeko la vituo 3,530, Zahanati zimeongezeka kutoka elfu 7,189 hadi elfu 8,706 huku hospitali zikiongezeka kutoka mia 404 hadi mia 475 mwaka 2026," amesema Waziri Mchengerwa

Aidha, Waziri Mchengerwa amesema Serikali imeongeza majengo mapya katika hospitali mbalimbali zikiwemo Hospitali ya Muhimbili, KCMC, BMH, Bugando, Mirembe, pamoja na Kibong'oto huku ikiwa imejenga hospitali mpya 10 za rufaa za mikoa, kukarabati hospitali kongwe 50, kukamilisha maboma 980 ya zahanati na kujenga vituo vya afya 390.

Amesema, katika huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto, Serikali imeongeza wodi za watoto wachanga kutoka 80 hadi 438 pamoja na vituo vya upasuaji wa dharura kutoka 445 hadi 630 ambayo ni mafanikio yaliyochangia kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 556 mwaka 2016 hadi vifo 104 mwaka 2022 kwa kila vizazi hai 100,000.

"Katika huduma za uchunguzi na matibabu ya kibingwa, Serikali imenunua na kusimika vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi bilioni 241.6 ambapo mashine za MRI zimeongezeka kutoka 7 hadi 13, CT Scan kutoka 12 hadi 45 pamoja na Digital X-ray kutoka 147 hadi 559," amesema Waziri Mchengerea

Kwa upande wa chanjo, amesema watoto waliopata chanjo ya Pentavalent dozi ya tatu wameongezeka kutoka watoto milioni 2,093,412 hadi milioni 3,186,979 huku kiwango cha chanjo kikiongezeka kutoka asilimia 93 hadi 96, juu ya lengo la kimataifa la asilimia 90.

"Upatikanaji wa dawa na

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share