02/09/2026
MWANAMKE MWENYE UMRI WA MIAKA 23 ATOLEWA UVIMBE WENYE KILO 12 KWENYE KIZAZI
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imefanikiwa kufanya upasuaji wa kuondoa uvimbe wenye uzito wa takribani kilo 12 kwenye kizazi cha mwanamke mwenye umri wa miaka 23 uliomtesa kwa muda mrefu.
Akizungumza wakati wa upasuaji huo Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Kinamama na Afya ya Uzazi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Musa Stambuli amesema kuwa uvimbe huo ulikuwa kwenye mayai ya upande wa kulia ambao umemtesa kwa zaidi ya miaka miwili.
Akuzungumzia kuhusu dalili za uvimbe huo amesema kuwa dalili za uvimbe huo mara nyingi zinafanana na zile za mfumo wa chakula ambapo mgonjwa anaweza kuhisi tumbo kujaa kila wakati, kupata maumivu ya mara kwa mara ya tumbo, kupata haja ndogo na kubwa mara kwa mara au kushindwa kupata haja kubwa k**a kawaida.
Pamoja na hayo ameongeza kuwa ni vyema mtu anapoona dalili hizo kuwahi hospitali kufanyiwa uchunguzi ili kubaini chanzo cha uvimbe huo kwa kuwa endapo tu atachelewa anaweza kupelekea kupata saratani ya kizazi