MNH-Mloganzila

MNH-Mloganzila Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MNH-Mloganzila, Medical and health, Kibamba, Dar es Salaam.

07/09/2026

“CT Scan ni mashine kubwa inayotumia mionzi ya X-ray kuchakata picha za ndani ya mwili, ambazo husaidia wataalamu wa afya kufanya uchunguzi na kubaini magonjwa mbalimbali”.

Dkt. Henry Malique
Daktari Bingwa wa Radiolojia
MNH-Mloganzila Muhimbili Taifa Wizara Ya Afya Elimu Ya Afya Kwa Umma

05/09/2026

“Mume wangu alipata kiharusi miezi mitano iliyopita, ambapo mkono wake ulikuwa hauwezi kuinuka wala kufanya kazi, baada ya kupata tiba kwa njia ya vitendo kwa sasa anaweza kutumia mkono wake. Kwakweli nawahamasisha wenye changamoto za kiharusi au ajali kutokata tamaa matibabu yanapatikana hospitalini”.

Bi. Anna Mtauka
Shuhuda wa huduma
MNH-Mloganzila. Elimu Ya Afya Kwa Umma Muhimbili Taifa Wizara Ya Afya

05/09/2026

“Mume wangu alipata kiharusi miezi mitano iliyopita, ambapo mkono wake ulikuwa hauwezi kuinuka wala kufanya kazi, baada ya kupata tiba kwa njia ya vitendo kwa sasa anaweza kutumia mkono wake. Kwakweli nawahamasisha wenye changamoto za kiharusi au ajali kutokata tamaa matibabu yanapatikana hospitalini”.

Bi. Anna Mtauka
Shuhuda wa huduma
MNH-Mloganzila Elimu Ya Afya Kwa Umma Muhimbili Taifa Wizara Ya Afya

MOI YAFANYA ZIARA MUHIMBILI, YAJIFUNZA UBUNIFU NA TEKNOLOJIA YA KISASA KATIKA KUTOA HUDUMAWataalam kutoka Taasisi ya Tib...
04/09/2026

MOI YAFANYA ZIARA MUHIMBILI, YAJIFUNZA UBUNIFU NA TEKNOLOJIA YA KISASA KATIKA KUTOA HUDUMA

Wataalam kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) wamefanya ziara ya kimkakati katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Upanga na Mloganzila, kwa lengo la kujifunza uzoefu wa hospitali hiyo katika utoaji wa huduma za kibingwa na kibingwa bobezi.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Dkt. Julieth Magandi, amesema kuwa ziara hiyo imelenga kujifunza matumizi ya teknolojia za kisasa, ubunifu, pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya kutoa huduma za afya pamoja na kubadilisha uzoefu huku jopo hilo likipata fursa ya kujifunza mifumo mbalimbali ya kidijitali inayotumiwa na MNH kuboresha huduma .

Naye Mkurugenzi wa huduma za mifupa MOI, Dkt. Antony Assei, aliipongeza MNH kwa mapinduzi ya kiteknolojia na uboreshaji wa miundombinu. Alibainisha kuwa mafunzo waliyoyapata yatasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha utendaji kazi ndani ya taasisi yao.

Aidha wataalam hao wapepata fursa ya kutembelea na kujionea Mfumo wa kudhibiti foleni (Queue Management System), Dashibodi ya huduma za kitabibu (Clinical Dashboard),Mfumo wa miadi kwa njia ya mtandao (Online Appointment System) na Mifumo ya kisasa ya ufuatiliaji na uchunguzi wa wagonjwa inayotumia Akili Mnemba (Artificial Intelligence - AI).

MAUMIVU MAKALI YA MAPAFU YATAJWA KUWA MOJA YA  DALILI YA KUJAA MAJI KWENYE MAPAFUImeelezwa kuwa tatizo la maji kuzunguka...
03/09/2026

MAUMIVU MAKALI YA MAPAFU YATAJWA KUWA MOJA YA DALILI YA KUJAA MAJI KWENYE MAPAFU

Imeelezwa kuwa tatizo la maji kuzunguka mapafu inaweza kusababisha ugumu wa kupumua na kuhusishwa na magonjwa mbalimbali ya mapafu, moyo, saratani au maambukizi.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya ndani kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Ivon Nyamahanga amesema ni muhimu mtu mwenye dalili hizo kufika kituo cha afya kwa uchunguzi kwani hali hiyo inaweza kujitokeza kwa dalili k**a upungufu wa pumzi, maumivu ya kifua, kikohozi na uchovu uliokithiri.

Kwa mujibu wa Dkt. Nyamahanga tatizo hilo huwakumba vijana na wazee ambapo katika Kliniki ya mapafu wagonjwa wenye changamoto hizo kwa siku huwa kati ya 3-4 huku visababishi vya tatizo hilo ikiwa ni kifua kikuu, homa ya mapafu, saratani, matatizo ya moyo, matatizo ya figo na matatizo ya ini.

Amesema matibabu hutegemeana na sababu iliyosababisha hali hiyo ambapo uchunguzi unaweza kuhusisha vipimo mbalimbali, ikiwemo picha ya kifua na vipimo vingine kulingana na hali ya mgonjwa.

Amesisitiza kuwa endapo mgonjwa hatotibiwa kwa wakati maji yataendelea kujaa na kukandamiza mapafu kiasi na kusababisha mgonjwa kukosa hewa na baadaye pafu linaweza kusinyaa na kushindwa kabisa kutanuka (total lung collapse) ambapo maji yanaweza kubadilika na kuwa usaha endapo yatapata maambukizi. Elimu Ya Afya Kwa Umma Wizara Ya Afya Muhimbili Taifa

MAUMIVU MAKALI YA MAPAFU YATAJWA KUWA MOJA YA  DALILI YA KUJAA MAJI KWENYE MAPAFUImeelezwa kuwa tatizo la maji kuzunguka...
03/09/2026

MAUMIVU MAKALI YA MAPAFU YATAJWA KUWA MOJA YA DALILI YA KUJAA MAJI KWENYE MAPAFU

Imeelezwa kuwa tatizo la maji kuzunguka mapafu inaweza kusababisha ugumu wa kupumua na kuhusishwa na magonjwa mbalimbali ya mapafu, moyo, saratani au maambukizi.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya ndani kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Ivon Nyamahanga amesema ni muhimu mtu mwenye dalili hizo kufika kituo cha afya kwa uchunguzi kwani hali hiyo inaweza kujitokeza kwa dalili k**a upungufu wa pumzi, maumivu ya kifua, kikohozi na uchovu uliokithiri.

Kwa mujibu wa Dkt. Nyamahanga tatizo hilo huwakumba vijana na wazee ambapo katika Kliniki ya mapafu wagonjwa wenye changamoto hizo kwa siku huwa kati ya 3-4 huku visababishi vya tatizo hilo ikiwa ni kifua kikuu, homa ya mapafu, saratani, matatizo ya moyo, matatizo ya figo na matatizo ya ini.

Amesema matibabu hutegemeana na sababu iliyosababisha hali hiyo ambapo uchunguzi unaweza kuhusisha vipimo mbalimbali, ikiwemo picha ya kifua na vipimo vingine kulingana na hali ya mgonjwa.

Amesisitiza kuwa endapo mgonjwa hatotibiwa kwa wakati maji yataendelea kujaa na kukandamiza mapafu kiasi na kusababisha mgonjwa kukosa hewa na baadaye pafu linaweza kusinyaa na kushindwa kabisa kutanuka (total lung collapse) ambapo maji yanaweza kubadilika na kuwa usaha endapo yatapata maambukizi. Wizara Ya Afya Elimu Ya Afya Kwa Umma Muhimbili Taifa

MAUMIVU MAKALI YA MAPAFU YATAJWA KUWA MOJA YA  DALILI YA KUJAA MAJI KWENYE MAPAFUImeelezwa kuwa tatizo la maji kuzunguka...
03/09/2026

MAUMIVU MAKALI YA MAPAFU YATAJWA KUWA MOJA YA DALILI YA KUJAA MAJI KWENYE MAPAFU

Imeelezwa kuwa tatizo la maji kuzunguka mapafu inaweza kusababisha ugumu wa kupumua na kuhusishwa na magonjwa mbalimbali ya mapafu, moyo, saratani au maambukizi.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya ndani kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Ivon Nyamahanga amesema ni muhimu mtu mwenye dalili hizo kufika kituo cha afya kwa uchunguzi kwani hali hiyo inaweza kujitokeza kwa dalili k**a upungufu wa pumzi, maumivu ya kifua, kikohozi na uchovu uliokithiri.

Kwa mujibu wa Dkt. Nyamahanga tatizo hilo huwakumba vijana na wazee ambapo katika Kliniki ya mapafu wagonjwa wenye changamoto hizo kwa siku huwa kati ya 3-4 huku visababishi vya tatizo hilo ikiwa ni kifua kikuu, homa ya mapafu, saratani, matatizo ya moyo, matatizo ya figo na matatizo ya ini.

Amesema matibabu hutegemeana na sababu iliyosababisha hali hiyo ambapo uchunguzi unaweza kuhusisha vipimo mbalimbali, ikiwemo picha ya kifua na vipimo vingine kulingana na hali ya mgonjwa.

Amesisitiza kuwa endapo mgonjwa hatotibiwa kwa wakati maji yataendelea kujaa na kukandamiza mapafu kiasi na kusababisha mgonjwa kukosa hewa na baadaye pafu linaweza kusinyaa na kushindwa kabisa kutanuka (total lung collapse) ambapo maji yanaweza kubadilika na kuwa usaha endapo yatapata maambukizi. Muhimbili Taifa Elimu Ya Afya Kwa Umma Wizara Ya Afya

02/09/2026

“Umuhimu wa kuimarisha huduma za afya ya msingi (Primary Health Care) ni nguzo muhimu ya kuboresha afya za wananchi na kufikia huduma za afya kwa wote (Universal Health Coverage)”.

Prof. Donatus Mutasingwa
Mkuu wa taaluma kitoka Chuo Kikuu cha Toronto chini Canada. Muhimbili Taifa Wizara Ya Afya

01/09/2026

Fahamu kuhusu kipimo cha Spirometry na jinsi kinavyotumika kupima uwezo wa mapafu namna unavyofanya kazi .

Ungana na Bw. Abel Thomas
Mtaalam wa vipimo vya mapafu
MNH- Mloganzila. Muhimbili Taifa Wizara Ya Afya Elimu Ya Afya Kwa Umma

JAMII YAKUMBUSHWA UMUHIMU WA KUTUNZA AFYA YA UBONGO, UTI WA MGONGO NA MISHIPA YA FAHAMUJamii imetakiwa kuchukua hatua za...
31/08/2026

JAMII YAKUMBUSHWA UMUHIMU WA KUTUNZA AFYA YA UBONGO, UTI WA MGONGO NA MISHIPA YA FAHAMU

Jamii imetakiwa kuchukua hatua za kulinda afya ya ubongo, uti wa mgongo na mishipa ya fahamu, kutokana na umuhimu wa viungo hivyo katika uwezo wa mtu kufikiri, kutembea, kuzungumza na kufanya shughuli mbalimbali za kila siku.

Rai hiyo imetolewa na Daktari Bingwa Mbobezi wa Magonjwa ya Ubongo, Uti wa Mgongo na Mishipa ya Fahamu kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Kigocha Okeng’o, ambaye amesema utunzaji wa mfumo wa fahamu ni muhimu kwa afya na ustawi wa mtu kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Dkt. Okeng’o ulaji wa lishe bora, kufanya mazoezi mara kwa mara, kupata usingizi wa kutosha pamoja na kudhibiti magonjwa k**a shinikizo la damu na kisukari, ni miongoni mwa hatua zinazoweza kusaidia kulinda afya ya ubongo na mfumo wa fahamu.

Amesisitiza pia umuhimu wa kuzuia majeraha ya kichwa na uti wa mgongo kwa kuzingatia kanuni za usalama barabarani, ikiwemo matumizi sahihi ya helmeti kwa waendesha pikipiki na baiskeli, pamoja na mikanda ya usalama kwa watumiaji wa magari.

Ameeleza kuwa, jamii inapaswa pia kuzingatia usalama katika maeneo ya kazi na wakati wa kufanya shughuli mbalimbali ili kupunguza uwezekano wa kupata majeraha yanayoweza kuathiri ubongo, uti wa mgongo au mishipa ya fahamu.

Aidha, amewataka wananchi kutopuuza dalili za hatari zinazoweza kuashiria tatizo katika mfumo wa fahamu, zikiwemo ganzi, udhaifu wa mwili, matatizo ya kuzungumza au kuona, kupoteza usawa pamoja na maumivu makali ya kichwa yanayoanza ghafla.

Amesema kutafuta huduma ya afya mapema mara tu dalili hizo zinapotokea ni muhimu katika kusaidia kutambua tatizo na kuanza matibabu kwa wakati. Muhimbili Taifa Wizara Ya Afya Elimu Ya Afya Kwa Umma

Address

Kibamba
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MNH-Mloganzila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MNH-Mloganzila:

Shortcuts

Share