MNH-Mloganzila

MNH-Mloganzila Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MNH-Mloganzila, Medical and health, Kibamba, Dar es Salaam.

06/06/2026

Kuelekea Siku ya Mchangia Damu Duniani, tarehe 14 Juni.

“Tone Moja la Ubinadamu, Changia Damu, Okoa Maisha.”

05/06/2026

05/06/2026
04/06/2026

Je! Unafahamu umuhimu wa matibabu ya Tiba Chemia (Chemotherapy) kwa mgonjwa wa saratani?

Ungana na Muuguzi Bingwa Magonjwa ya Saratani kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Bi. Sekuye Moshi kwa ufafanuzi zaidi.

03/06/2026

“Hongera Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila na timu nzima ya wataalamu wa afya kwa mafanikio ya huduma ya Immediate Kangaroo Mother Care (IKMC), hatua muhimu inayookoa maisha ya watoto wachanga.”
Dkt. Mariam Johari, Mkurugenzi wa program ya NEST360 Tanzania.

WAFANYAKAZI  BORA 45 WATUNUKIWA VYETI MUHIMBILI MLOGANZILA.Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila imewapongeza na kuwat...
02/06/2026

WAFANYAKAZI BORA 45 WATUNUKIWA VYETI MUHIMBILI MLOGANZILA.

Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila imewapongeza na kuwatambua wafanyakazi bora 45, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utendaji kazi wenye tija na utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila Dkt. Julieth Magandi amesema wafanyakazi waliotambuliwa wamefanikiwa kukidhi vigezo, ikiwemo kupata angalau asilimia 75 katika tathmini ya utendaji kazi kupitia Mfumo wa PEPMIS.

Dkt. Magandi amefafanua kuwa mafanikio hayo yanaonesha dhamira yao ya dhati katika kuimarisha huduma za afya na kufanikisha malengo ya hospitali.

Amesema utaratibu wa kutambua na kuwazawadia wafanyakazi bora unalenga kuongeza motisha kwa watumishi, kuimarisha utamaduni wa uwajibikaji na kuhamasisha wafanyakazi wengine kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufikia viwango vya juu vya utoaji huduma.

02/06/2026

“Mgonjwa yeyote ambaye anachangamoto kwenye mfumo wa mkojo iliyozoeleka kuitwa UTI sugu anahitaji kufanya vipimo zaidi kujidhihirisha k**a hana Saratani ya kibofu cha mkojo”.

Dkt. David Mgaya, Daktari Bingwa wa Upasuaji Mfumo wa Mkojo na Bobezi Magonjwa ya Afya ya Uzazi kwa Wanaume Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila.

01/06/2026

“Baada ya kufanyiwa uchunguzi wa CT-Scan, niligundulika kuwa na uvimbe ndani ya kibofu cha mkojo. Wataalamu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila walinipokea na kunipatia huduma za kibingwa kwa weledi mkubwa, ambapo nilifanyiwa upasuaji kwa mafanikio. Kwa sasa afya yangu imeimarika. Nawashukuru sana Wataalamu kwa huduma bora na ukarimu.”

Bw. Cosmas Makoye,
Shuhuda wa huduma,
Chalinze.

MNH-MLOGANZILA YAWAHAMASISHA WANANCHI KUZIJUA NAMBA ZAO KUPITIA UCHUNGUZI WA AFYAHospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila...
30/05/2026

MNH-MLOGANZILA YAWAHAMASISHA WANANCHI KUZIJUA NAMBA ZAO KUPITIA UCHUNGUZI WA AFYA

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kufanya uchunguzi wa afya kupitia kampeni ya “Zijue Namba Zako” iliyofanyika katika viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kupambana na magonjwa yasiyoambukiza.

Kupitia kampeni hiyo, wananchi wamepata huduma za uchunguzi wa afya ikiwemo upimaji wa urefu, uzito, kipimo cha uzito kulingana na urefu (BMI) pamoja na kiwango cha sukari kwenye damu, hatua inayowasaidia kutambua hali zao za afya mapema na kuchukua hatua stahiki kabla ya madhara ya magonjwa yasiyoambukiza kuongezeka.

Sambamba na huduma za uchunguzi, wataalamu kutoka MNH-Mloganzila wametoa elimu kuhusu kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza pamoja na matumizi sahihi ya bima ya afya, huku wakihamasisha wananchi kujenga utamaduni wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara kwa ajili ya kulinda afya zao.

Huduma hiyo imetolewa katika kampeni ya Ongea na Waziri wa Afya, jukwaa lililowawezesha wananchi pia kutoa maoni, kuuliza maswali na kuwasilisha changamoto mbalimbali zinazohusu huduma za afya kwa lengo la kupata majibu na ufumbuzi wa kudumu.

Kupitia kampeni ya “Zijue Namba Zako,” MNH-Mloganzila imeendelea kusisitiza umuhimu wa uchunguzi wa mapema k**a hatua muhimu ya kinga na udhibiti wa magonjwa yasiyoambukiza katika jamii.

30/05/2026

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali kupambana na Magonjwa yasiyoambukiza, Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila imeshiriki kutoa huduma za dharura, uchunguzi wa afya na ushauri katika tukio la Ongea na Waziri wa Afya viwanja vya posta Kijitonyama.
Kupitia huduma hiyo, wananchi wataweza kutoa maoni, kuuliza maswali, na kuwasilisha malalamiko ambayo yatafuatiliwa hadi kupatiwa majibu au ufumbuzi wa kudumu.

Address

Kibamba
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MNH-Mloganzila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MNH-Mloganzila:

Share