11/01/2026
*📘 SOMO: UGONJWA WA TEZI DUME*
*Na Dkt. Steven Hinjo – Tabibu wa Tiba Asilia na Tiba Lishe*
---
🔹 *TEZI DUME NI NINI?*
Tezi dume (Prostate) ni kiungo kidogo kilichopo chini ya kibofu cha mkojo kwa wanaume. Inazalisha majimaji yanayosaidia mbegu za kiume. Ugonjwa wa tezi dume hutokea inapovimba au kuwa na uvimbe usio wa kawaida.
---
🧪 *SABABU ZA UGONJWA WA TEZI DUME*
1. *Kuongezeka kwa umri (zaidi ya miaka 45)*
2. *Mabadiliko ya homoni*
3. *Kurithi (genetics)*
4. *Lishe isiyo bora – yenye mafuta mengi na nyama nyekundu*
5. *Kutofanya mazoezi*
6. *Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe*
7. *Msongo wa mawazo (stress)*
---
⚠️ *DALILI ZA AWALI (HATUA YA KWANZA)*
- Kukojoa mara kwa mara hasa usiku
- Mkojo kutoka kwa shida au kudondoka
- Maumivu au hisia ya kuungua wakati wa kukojoa
- Kukosa nguvu za kiume kwa baadhi ya wanaume
---
⚠️ *DALILI ZA HATUA YA PILI*
- Mkojo kujaa bila kutoka vizuri
- Maumivu ya nyonga na mgongo wa chini
- Mkojo kuwa na damu
- Kuhisi haja ya kukojoa lakini mkojo hautoki
---
⚠️ *DALILI ZA HATUA YA TATU*
- Kushindwa kabisa kukojoa (retention)
- Maumivu makali kwenye nyonga na mifupa
- Kushuka kwa uzito
- Uchovu kupita kiasi
- Kuvuja damu mara kwa mara kwenye mkojo au manii
---
❗*MADHARA K**A HAITATIBIWA- Uharibifu wa kibofu cha mkojo
- Maambukizi ya mara kwa mara (UTI)
- Kushindwa kabisa kukojoa
- Uharibifu wa figo
- Saratani ya tezi dume (Prostate Cancer)
---
❌ *VITU VYA KUEPUKA*
- Pombe na sigara
- Vyakula vyenye mafuta mengi
- Nyama nyekundu kwa wingi
- Uvivu wa kufanya mazoezi
- Msongo wa mawazo
- Kukaa muda mrefu bila shughuli
---
✅ *VYAKULA NA VINYWAJI VYA KUTUMIA*
- Parachichi
- Mbegu za maboga (pumpkin seeds)
- Matunda k**a tikiti, zabibu, ndizi
- Samaki wa mafuta (k**a salmon)
- Mboga za majani (spinach, broccoli, kabeji)
- Tangawizi, kitunguu saumu
- Unga wa *amla*, *karafuu*, *tangawizi*, *moringa*, n.k.
- Juisi ya miwa, juisi ya beetroot
- Maji mengi kila siku (lita 2–3)
---
*💬 USHAURI WA DR. HINJO:*
Kagua afya ya tezi dume mara kwa mara baada ya miaka 45. Tumia lishe bora na tiba asilia zenye kuthibiti homoni na kupunguza uvimbe wa tezi. Kwa ushauri na huduma, karibu kwenye vituo vyetu.
📞 *Dr. Steven Hinjo*
☎️ 0652 200200 | 0626 709700
📍 *Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Tanga*
---
*“Afya ni msingi wa furaha, linda tezi dume mapema.”*