Dr Abduly Kisalazo

Dr Abduly Kisalazo TUNATOA HUDUMA ZA AFYA

JINSI YA KUPUNGUZA HATARI YA KUPATA UGONJWA WA KISUKARI.Kisukari ni ugonjwa hatari ambao unaweza kusababisha madhara mak...
31/03/2025

JINSI YA KUPUNGUZA HATARI YA KUPATA UGONJWA WA KISUKARI.

Kisukari ni ugonjwa hatari ambao unaweza kusababisha madhara makubwa kwa afya yako.

Kwa bahati mbaya, idadi ya watu wanaougua kisukari inaongezeka kila mwaka, hivyo ni muhimu kuchukua hatua za kuzuia ugonjwa huu mapema kabla ya kujitokeza

Idadi ya watu wenye Ugonjwa wa Kisukari(diabetes) Duniani iliongezeka kutoka Million108 mwaka1980 mpaka kufikia Watu million 422 kwa mwaka 2014, Je k**a Idadi inaongezeka kila mwaka leo hali Ipoje?

Pia ugonjwa huu wa Kisukari ni chanzo kikubwa cha matatizo mengine k**a vile;

● Upofu wa macho(blindness),

● Tatizo la Figo kushindwa ●kufanya kazi(kidney failure),

● Shambulio la moyo(heart attacks),

● Tatizo la kiharusi(stroke)

● Pamoja na Tatizo la watu Kukatwa MIGUU

📌 Kuna hatua kadhaa za kufuata ili kupunguza hatari ya kupata kisukari, na makala hii itakusaidia kujifunza jinsi ya kufanya hivyo.

1.Punguza au Acha kula vyakula vya wanga au carbohydrates. (Vyakula vilivyo kobolewa )

Vyakula vyenye kiwango cha juu cha sukari, wanga, na mafuta yasiyofaa ni hatari kwa afya yako na vinaweza kuongeza hatari ya kupata kisukari.

Kwa hiyo, ni muhimu kuzingatia ulaji wa vyakula sahihi, k**a vile matunda, mboga mboga za majani, protini, na wanga unaochujwa.

2. Fanya Mazoezi ya mara kwa mara

Mazoezi ya mara kwa mara yanasaidia kupunguza hatari ya kupata kisukari,

Jaribu kufanya mazoezi kwa angalau dakika 30 kwa siku, angalau siku tano kwa wiki.

Mfano wa mazoezi haya ni pamoja na

●Mazoezi ya kutembea,

●kukimbia,

●kuogelea,

●Kuendesha baiskeli,

●Pamoja na yoga.

3. Punguza Unene wa mwili

Unene wa mwili ni hatari kwa afya yako na inaweza kuongeza hatari ya kupata kisukari. Kwa hiyo, ni muhimu kupunguza uzito wako kwa kupitia lishe bora na mazoezi ya mara kwa mara.

4. Tumia Maji ya kutosha

Unywaji wa maji wa kutosha ni muhimu kwa afya yako na inaweza kusaidia kupunguza hatari ya kupata kisukari. Jaribu kunywa angalau lita 2.5 ya maji kwa siku.

5. Punguza Matumizi ya Pombe

Matumizi ya pombe ni hatari kwa afya yako na inaweza kuongeza hatari ya kupata kisukari. Kwa hiyo, ni muhimu kupunguza matumizi ya pombe au kuepuka kabisa matumizi yake.

✍️Ni muhimu kufuata hatua hizi k**a njia ya kudumu ili kuhakikisha afya yako na kuepuka hatari ya kupata kisukari.

🥦K**a umeshapata ugonjwa huu upate tiba za mimea asilia zenye uwezo wa kushusha sukari na kuwa katika kiwango sahihi kinachotakiwa

KWA USHAURI NA TIBA JUU YA CHANGAMOTO YA KISUKARI TUWASILIANE KWA NAMBA 0741438383

TIBA YA ACID REFLUX MEPATIKANA MSHAURI MAKINI, DR. Dr Abduly Kisalazo  ZIJUE DALILI ZA ACID REFLUX• Mchomo au maumivu ka...
31/03/2025

TIBA YA ACID REFLUX MEPATIKANA
MSHAURI MAKINI, DR. Dr Abduly Kisalazo

ZIJUE DALILI ZA ACID REFLUX

• Mchomo au maumivu katika tumbo, 1-4 masaa baada ya mlo
• maumivu ya kifua
• Kiungulia cha Muda mrefu
• Uvimbe katika kifua
• Kuhisi njaa mara kwa mara
• Daima maumivu katika tumbo la juu
• Kucheua
• Kichefuchefu
• Kuona Uchungu ladha katika kinywa
• Kupoteza hamu ya kula
• Kutapika
• Kukohoa
• Sauti ya mabadiliko na malezi ya kidonda katika umio (tube kuunganisha kinywa na tumbo)
• Maumivu ya sehemu za misuli ya mwili

SABABU ZA ACIDITY
• Uvutaji wa sigara kwa wingi
• Kunywa pombe kupita kiasi
• Vidonda vya tumbo
• kuzidi kwa asidi ya tumbo
• Kutokula kwa wakati
• Kula kukaanga na viungo vya chakula mara kwa mara
• Matatizo katika utendaji wa mfumo wa mmeng'enyo wa chakula tumboni
• Kukaa na njaa kwa muda mrefu au kuto kula chakula cha Asubuhi
• Kula vyakula vingi vya mafuta, k**a chocolates
• kuwa na Mimba kunasababisha asidi pia.
• kuzeeka
• Utokaji yatokanayo na jua na joto
• Muafaka wa chakula tabia
• kuwa hisia mbaya
• Udhaifu wa mishipa ya mwilini

TUNATIBU ACID REFLUX INAYO SABABISHA VIDONDA VYA TUMBO. TUNATIBU VIDONDA VYA TUMBO NDANI YA SIKU 15

➡️DISCOUNT YA MSIMU HUU WA SIKUKUU
GHARAMA YA MATIBABU NI TSH 69,000/= BADALA YA 120,000/=

TIBA INAPATIKANA NA MATOKEO NI KWANZIA SIKU TANO TIBA NI YA SIKU 15
UNAHITAJI TIBA PIGA SIMU
USISUBIRI MAUMIVU YAWE MAKUBWA TIBU MAPEMA UPONE MAPEMA

KWA USHAURI NA TIBA
0741438383

𝗞𝗪𝗔𝗡𝗜𝗡𝗜 𝗜𝗡𝗜 𝗟𝗘𝗡𝗬𝗘 𝗞𝗢𝗩𝗨 𝗡𝗜𝗥𝗔𝗛𝗜𝗦𝗜 𝗞𝗨𝗕𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗞𝗔 𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗙𝗜𝗞𝗜𝗔 𝗦𝗧𝗔𝗚𝗘 𝗬𝗔 𝗦𝗔𝗥𝗔𝗧𝗔𝗡𝗜Ini lenye maambukizi ya hepatitis linaweza kuwa n...
31/03/2025

𝗞𝗪𝗔𝗡𝗜𝗡𝗜 𝗜𝗡𝗜 𝗟𝗘𝗡𝗬𝗘 𝗞𝗢𝗩𝗨 𝗡𝗜𝗥𝗔𝗛𝗜𝗦𝗜 𝗞𝗨𝗕𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗞𝗔 𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗙𝗜𝗞𝗜𝗔 𝗦𝗧𝗔𝗚𝗘 𝗬𝗔 𝗦𝗔𝗥𝗔𝗧𝗔𝗡𝗜

Ini lenye maambukizi ya hepatitis linaweza kuwa na hatari kubwa ya kubadilika kuwa saratani kwa sababu ya mabadiliko ya kimetaboliki yanayotokea katika ini wakati wa maambukizi. Hepatitis, hasa aina ya B na C, inaweza kusababisha kuvimba kwa ini kwa muda mrefu, na baada ya muda, hii inaweza kusababisha uharibifu wa seli za ini na kuongeza hatari ya kupata saratani ya ini (Hepatocellular carcinoma).

Sababu kuu zinazochangia hili ni:

1. Mabadiliko ya DNA: Hepatitis huleta mabadiliko katika DNA ya seli za ini. Hii inaweza kusababisha seli za ini kugawanyika vibaya au kuendelea kugawa bila udhibiti, jambo ambalo linahusiana na maendeleo ya saratani.

2. Fibrosis na Cirrhosis: Maambukizi ya hepatitis yanaweza kusababisha fibrosis (makovu kwenye ini) na hatimaye cirrhosis (uharibifu mkubwa wa ini). Ini lenye cirrhosis lina uwezekano mkubwa wa kuwa na saratani kwa sababu ya ukuaji wa seli zisizo za kawaida.

3. Inflammation ya muda mrefu: Maambukizi ya hepatitis husababisha uchochezi wa muda mrefu kwenye ini. Uchochezi huu unaweza kusababisha madhara ya kimetaboliki, ambayo husababisha mabadiliko ya seli na hatimaye saratani.

Kwa hiyo, ikiwa mtu ana maambukizi ya hepatitis na ana kovu kwenye ini, ni muhimu kuwa na uangalizi wa kiafya na kufuata matibabu ili kupunguza hatari ya maendeleo ya saratani. Matibabu yanaweza kujumuisha antivirals kwa hepatitis B na C, na hatua za kudhibiti cirrhosis au fibrosis.

Wasiliana nasi kupitia namba +255 0741438383

JE? WAJUAInawezekana umetumia bidhaa nyingi za mifupa ,umefanya mazoezi, umefanya masaji na umetuma pesa nyingi ujapata ...
31/03/2025

JE? WAJUA
Inawezekana umetumia bidhaa nyingi za mifupa ,umefanya mazoezi, umefanya masaji na umetuma pesa nyingi ujapata matokeo!!!! Hivi umewai kujiuliza Kwa nini MPAKA sasa ujapona??? Watu WENGI wamekua wakitibu maumivu TU . Hawatibu chanzo Cha tatizo hivyo kupelekea maumivu kujirudia rudia, na kukata tamaa .
Hivo basi PATA suluhisho la kudumu la kutatua changamoto yako ya mifupa bila upasuaji Kwa kutumia virutubisho lishe vilivyoweza kusaidia watu WENGI na wamepona kabisa

0741 438 383

Kwa kutumia package inayosaidia
1.kutengeneza Ute Ute Ili kurudisha mjongeo wa mifupa
2.kuzuia mifupa au pingili kusagika
3.kuponya majeraha na maumivu ya mgongo, nyonga, magoti n.k
4.huzalisha madini k**a calcium, magnesium, zinc, seleun, potassium Ili kuimarisha mifupa
5.huzuia misuli kuuma au kukaza
6.huondoa changamoto ya ganzi na
kuwakaa moto sehemu za miguu na mikono
7.dose hii ukitumia huna haja ya kufanyiwa upasuaji

* BEI YA DOSE NI KUTOKANA NA TATIZO LAKO DAWA ZIPO KATIKA MFUMO WA VIDONGE*
Dr Abduly Kisalazo +255741438383

Vidonda vya tumbo na asidi nyingi (acid reflux) ni matatizo yanayoweza kuathiri mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Vidonda ...
24/03/2025

Vidonda vya tumbo na asidi nyingi (acid reflux) ni matatizo yanayoweza kuathiri mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Vidonda vya tumbo husababishwa na kuharibika kwa kuta za tumbo kutokana na asidi kali, wakati asidi nyingi husababisha kiungulia na kurudi kwa asidi kwenye umio (GERD).

Dalili za Vidonda vya Tumbo na Asidi Nyingi

Maumivu ya tumbo (hasa sehemu ya juu katikati)

Kiungulia na hisia ya moto kifuani

Tumbo kujaa gesi na kubanwa

Kichefuchefu au kutapika

Kukosa hamu ya kula

Njia za Kupunguza Asidi na Vidonda vya Tumbo

1. Lishe Bora

Kula vyakula vyenye alkali: Mboga za majani, ndizi, matunda k**a tikiti maji na papai.

Epuka vyakula vyenye asidi nyingi: Vyakula vya kukaanga, pilipili, nyanya, kahawa, soda, pombe, na vyakula vyenye viungo vikali.

Kula mara kwa mara kwa kiasi kidogo: Badala ya milo mikubwa, kula mara 5-6 kwa siku.

2. Vinywaji vya Kusaidia

Maji ya uvuguvugu: Husaidia kupunguza mkusanyiko wa asidi tumboni.

Juisi ya kiazi mviringo mbichi: Ina alkali inayopunguza asidi.

Juisi ya aloe vera: Inasaidia kutuliza kuta za tumbo.

3. Mtindo wa Maisha

Epuka kulala mara baada ya kula: Subiri angalau saa 2-3 kabla ya kulala.

Inua mto unapolala: Kuweka kichwa juu husaidia asidi isirudi juu.

Epuka msongo wa mawazo: Stress inaweza kuongeza uzalishaji wa asidi tumboni.

Kwa ushauri na matibabu sahihi wasailana na DR ABDULY KISALAZO kupitia namba 0741438383

𝗙𝗔𝗛𝗔𝗠𝗨 𝗞𝗨𝗛𝗨𝗦𝗨 𝗠𝗔𝗔𝗠𝗕𝗨𝗞𝗜𝗭𝗜 𝗬𝗔 𝗩𝗜𝗥𝗨𝗦𝗜 𝗩𝗬𝗔 𝗛𝗢𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗜𝗡𝗜 [𝗛𝗘𝗣𝗔𝗧𝗜𝗧𝗜𝗦], 𝗡𝗝𝗜𝗔 𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗠𝗕𝗨𝗞𝗜𝗭𝗜, 𝗗𝗔𝗟𝗜𝗟𝗜 𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗧𝗜𝗕𝗔𝗕𝗨:Homa ya ini hujul...
15/03/2025

𝗙𝗔𝗛𝗔𝗠𝗨 𝗞𝗨𝗛𝗨𝗦𝗨 𝗠𝗔𝗔𝗠𝗕𝗨𝗞𝗜𝗭𝗜 𝗬𝗔 𝗩𝗜𝗥𝗨𝗦𝗜 𝗩𝗬𝗔 𝗛𝗢𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗜𝗡𝗜 [𝗛𝗘𝗣𝗔𝗧𝗜𝗧𝗜𝗦], 𝗡𝗝𝗜𝗔 𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗠𝗕𝗨𝗞𝗜𝗭𝗜, 𝗗𝗔𝗟𝗜𝗟𝗜 𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗧𝗜𝗕𝗔𝗕𝗨:

Homa ya ini hujulikana kwa kitaalamu k**a Hepatitis.

𝗛𝗲𝗽𝗮𝘁𝗶𝘁𝗶𝘀 ni kirusi kinacho sababisha ugonjwa mkali wa ini na saratani ya ini baada ya kuishi na maambukizi ya muda mrefu pasipo kutibiwa.

Katika maeneo yetu, bara la afrika maambukizi ya virusi vya homa ya ini ndio sababu kuu ya ugonjwa wa ini.

Virusi vya homa ya ini vipo vya aina 5 (A,B,C,D,E) ambapo aina mbili za virusi (B na C ) ndio sababu kuu za ugonjwa wa homa ya ini na husambaa kupitia damu na majimaji ya mwili k**a vile manii na Jasho.

𝗛𝗼𝗺𝗮 𝘆𝗮 𝗶𝗻𝗶 ni sawa janga linaloua kimya kimya kulingana na takwimu za vifo vya dunia inakadiriwa kirusi cha homa ya ini aina ya B pekee huua watu 600,000 hivi kila mwaka.

Kwa wastani zaidi ya watu bilioni mbili, yaani, asilimia 33 hivi ya watu wote ulimwenguni, wameambukizwa virusi vya HBV (Hepatitis B Virus), na wengi wao hupona baada ya miezi michache kupitia kinga zao za mwili au kupitia medications ya dozi za Ant-hepatitis B Virus.

Watu milioni 350 hivi huendelea kuwa na virusi hivyo mwilini, wengi huishi bila dalili na kuendelea kuambukiza watu wengine.

𝗕𝗔𝗔𝗗𝗛𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗝𝗜𝗔 𝗭𝗔 𝗞𝗨𝗦𝗔𝗠𝗕𝗔𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗠𝗕𝗨𝗞𝗜𝗭𝗜 𝗬𝗔 𝗩𝗜𝗥𝗨𝗦 𝗩𝗬𝗔 𝗛𝗢𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗜𝗡𝗜:

➖ Kushiliki ngono isiyo salama na mtu mwenye kuishi na maambukizi ya virus vya Hepatitis.

➖ Kuchangia vitu vyenye ncha kali k**a vile sindano, kisu NK.

➖ Kuvaliana na nguo na mtu mwenye maambukizi ya virus vya Hepatitis.

➖ Kushika maji maji yatokayo mwilini mwa mtu alie na maambukizi ya virus vya homa ya ini Hepatitis.

➖ Kuchangia damu au kutumia vifaa vya kusafishia damu k**a ilivyo kwa Dialysis ya figo.

𝗕𝗔𝗔𝗗𝗛𝗜 𝗬𝗔 𝗗𝗔𝗟𝗜𝗟𝗜 𝗭𝗔 𝗛𝗢𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗜𝗡𝗜:

Kwa kawaida dalili za mwanzo za homa ya ini hutokea ndani ya miezi 6 baada kuambukizwa,na hutokea kwa baadhi ya watu hazitokei kwa kila mtu.

Mgonjwa mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini hupata dalili zifuatazo;

➖ Tumbo kujaa Gesi, vidonda vya tumbo, uchovu na kuishiwa nguvu.

➖ Kichefuchefu na kutapika pamoja na kupoteza hamu ya kula

➖ Miwasho ya ngozi na majipu ya mara kwa mara.

➖ Homa kali na za mara kwa mara.

➖ Kupoteza hamu ya tendo la ndoa kwa jinsia zote.

➖ Kunenepa na kuongezeka uzito kupita kiasi kutokana na mrundikano wa mafuta na sumj kupita kiasi.

➖ Maumivu makali ya tumbo upande wa ini upande wa kulia.

➖ Macho na ngozi kuwa na rangi ya njano.

➖ Mkojo wa njano iliyo kolea, mweusi/mkojo kuwa na rangi iliyokolea k**a coca-cola.

𝗠𝗔𝗗𝗛𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗜𝗦𝗛𝗜 𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗠𝗕𝗨𝗞𝗜𝗭𝗜 𝗬𝗔 𝗩𝗜𝗥𝗨𝗦𝗜 𝗩𝗬𝗔 𝗛𝗢𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗜𝗡𝗜 𝗞𝗪𝗔 𝗠𝗨𝗗𝗔 𝗠𝗟𝗘𝗙𝗨 𝗣𝗔𝗦𝗜𝗣𝗢 𝗞𝗨𝗧𝗜𝗕𝗜𝗪𝗔:

Kuna kundi dogo la wagonjwa wa homa ya ini hupata ugonjwa mkali wa ini na kusababisha ini kushindwa kabisa kufanya kazi pia huweza kusababisha kifo. Hii hatua huitwa “𝗳𝘂𝗹𝗺𝗶𝗻𝗮𝗻𝘁 𝗹𝗶𝘃𝗲𝗿 𝗳𝗮𝗶𝗹𝘂𝗿𝗲”.

Watu wenye maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini mara nyingi huwa hawana dalili kwa miaka mingi, kadri muda unavyoenda virusi vya hepatitis husababisha ini kusinyaa hatua hii ya ini kusinyaa huitwa (𝗹𝗶𝘃𝗲𝗿 𝗰𝗶𝗿𝗿𝗵𝗼𝘀𝗶𝘀) hupelekea ini kushindwa kabisa kufanya kazi vyema.

Pia maambukizi ya virusi vya homa ya ini huchangia kupata saratani ya ini ambayo hujulikana kwa kitaalamu k**a 𝗵𝗮𝗽𝗮𝘁𝗼𝗰𝗲𝗹𝗹𝘂𝗹𝗮𝗿 𝗰𝗮𝗿𝗰𝗶𝗻𝗼𝗺𝗮.

𝗞𝗨𝗠𝗕𝗨𝗞𝗔: Watu wengi wameangaika katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili, ili kunusuru maisha kwa ghalama mbali mbali na hatimae kukosa kutimiza lengo la matibabu katika kumaliza tatizo hili na mwisho huishi na fikra potofu au tofauti ya kuamini kwamba ugonjwa huu hauna tiba na hivyo hupoteza matumaini ya kuendelea kuishi.

Ugonjwa huu unatibika kupitia dozi sahihi ya Hepatitis Ant-Viral uku ukizingatia lishe yenye manufaa kwa afya ya INI pamoja na seli zake, mazoezi na utumiaji wa matunda kwa wingi pamoja na mboga za majani.

Matibabu ya tatizo hili yanategemea pia na hatua ya tatizo lilipo fikia katika upande wa afya ya ini [Liver Demage] pamoja na wingi wa maambukizi, tatizo linaweza kuisha mapema na kupata chanjo ya kuzuiya kupata tena maambukizi ya virusi vya homa ya ini endapo utawai matibabu ya mapema kabla ya ini kufikia hatua mbaya ya kovu.

Sikuzote kovu la ini halitibiki na hii ndio sababu ya kwamba homa ya ini haina tiba unaweza ukatokomeza maambukizi na kupata chanjo lakini k**a ini tayari limesha kuwa na kovu inakuwa bado ni changamoto kwasababu kovu la ini ndio chanzo cha saratani ya ini:

0741 438 383

𝗞𝗪𝗔𝗞𝗨𝗭𝗜𝗡𝗚𝗔𝗧𝗜𝗔 𝗠𝗔𝗧𝗜𝗕𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔 𝗟𝗜𝗦𝗛𝗘 𝗕𝗢𝗥𝗔 𝗡𝗜 𝗛𝗔𝗧𝗨𝗔 𝗭𝗔 𝗠𝗦𝗜𝗡𝗚𝗜 - 𝗞𝗔𝗧𝗜𝗞𝗔 𝗞𝗨𝗧𝗢𝗞𝗢𝗠𝗘𝗭𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗠𝗕𝗨𝗞𝗜𝗭𝗜 𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗘𝗣𝗨𝗦𝗛𝗔 𝗛𝗔𝗧𝗔𝗥𝗜 𝗭𝗔 𝗦𝗜𝗞𝗨 𝗭𝗜𝗝𝗔𝗭𝗢:

𝗞𝗮𝗿𝗶𝗯𝘂 𝘁𝘂𝗸𝘂𝗵𝘂𝗱𝘂𝗺𝗶𝗲 𝗸𝘄𝗮 𝗰𝗵𝗮𝗻𝗴𝗮𝗺𝗼𝘁𝗼 𝘇𝗮 𝗮𝗳𝘆𝗮 𝘁𝘂𝗻𝗮𝘁𝗼𝗮 𝗵𝘂𝗱𝘂𝗺𝗮 𝘇𝗮 𝗩𝗜𝗣𝗜𝗠𝗢, 𝗨𝗦𝗛𝗔𝗨𝗥𝗜, 𝗠𝗔𝗧𝗜𝗕𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗡𝗝𝗢:

VINYWAJI AMBAVO MGONJWA WA SUKARI HATAKIWI KUTUMIA KABISANimekuwa nikipata maswali mara kwa mara ni kinywaji ambayo mgon...
13/03/2025

VINYWAJI AMBAVO MGONJWA WA SUKARI HATAKIWI KUTUMIA KABISA

Nimekuwa nikipata maswali mara kwa mara ni kinywaji ambayo mgonjwa wa sukari hatakiwi kutumia KABISA

Leo nimeamua kuandika makala ya vinywaji gani mgonjwa wa sukari hatakiwi kutumia kabisa

1. SODA: Hii haitaki mjadala mkubwa

Soda ina kiwango kikubwa cha sukari na carbohydrates ndani yake lakini pia soda haina fiber hivyo ukiinywa inaenda kupandisha sukari moja kwa moja

Achana na matumizi ya soda aina zote

2. Soda dayat: nimekuwa nikiiulizwa sana kuhusu soda diet

Kwa ufupi soda diet Haifai kwa mgonjwa wa sukari sababu wanaeka MSG (MONO SODIUM GLUTAMATE) ama inaitwa artificial sweetener

Haifai hata kidogo kwa mgonjwa wa sukari

3. Energy drinks: ni k**a ilivo soda energy drinks hazifai kwa mgonjwa wa sukari

4. Pombe: pombe aina zote hazifai kwa mgonjwa wa sukari

Wengine wanasema serengeti haina kiwango kikubwa cha sukari

Sikia pombe zote zinafanyiwa umengenywaji na ini

Na inazaa msururu wa sukari na mwishowe inasababisha fat liver ambayo ni chanzo kikubwa cha insulin resistance na mwishowe kisukari

Achana na pombe aina zote utakuja kunishukuru baadae

Je umefaidika na makala hii??

Comment kitu ambacho umejifunza

MATUMIZI YA DAWA WAKATI WA UJAUZITOMara kwa mara wanawake wengi hugundua kuwa ni wajawazito baada ya kukosa hedhi. Hivyo...
11/03/2025

MATUMIZI YA DAWA WAKATI WA UJAUZITO

Mara kwa mara wanawake wengi hugundua kuwa ni wajawazito baada ya kukosa hedhi. Hivyo ni vyema kutambua madhara ya madawa mbali mbali hata kabla hujafikiria kuwa mjamzito ili ujue nini cha kuepuka.

Dawa nyingi hazijafanyiwa majaribio k**a ni salama kwa ujauzito. Unachoweza kufanya kuepuka matatizo ni kuamua kutotumia dawa yoyote katika ujauzito wako labda tu uwe umeshauriwa na daktari.

Dawa mbali mbali zinaweza zikaathiri ukuaji wa mtoto wako kwa njia nyingi, ikiwemo:

👉Kubadilisha mazingira ya mji wa mimba hivyo kusababisa uhaba wa mahitaji muhimu kwa mtoto
👉Kubadilika kwa uwiano wa ukuaji sahihi wa mtoto hivyo kusababisha mtoto kuzaliwa njiti
👉Kusababisha kuzaliwa na matatizo au mimba kutoka
👉Kusababisha matatizo ya kupumua baada ya mtoto kuzaliwa

K**a unatumia dawa za aina yoyote ile na umegundua kuwa ni mjamzito ni vyema kuwasiliana na daktari wako mara moja kabla hujaacha kuzitumia kwani maisha yako yanaweza yakawa yanategemea dawa hizi. Daktari wako ataweza kukushauri kuhusu dawa unazotumia k**a ni salama au la kwenye ujauzuto na kukubadilishia kadiri itakavyoonekana ni sawa.

Ni vyema pia kuwa makini na dawa zinazoitwa za asili. Kwa sababu tu zimeandikwa ni dawa za asili haimaanishi hazina uwezo wa kuleta shida kwenye ujauzito wako. Dawa nyingi za asili pia zina uwezo wa kuleta matatizo kipindi cha ujauzito hivyo ni vyema kutokutumia dawa za asili ukiwa mjamzito.

Dawa yoyote ile ambayo utaitumia mwilini kwako kipindi cha ujauzito ni vyema iwe imetolewa na daktari wako anaetambua kwamba wewe ni mjamzito. Baadhi ya wanawake hununua dawa kwenye maduka ya dawa baridi k**a Paracetamol pale wanapohisi maumivu. Ni vyema pia kupata ushauri wa daktari kwani kuna baadhi ya dawa za maumivu unaweza ukawa unahisi ni salama (kwani si za maumivu tuu), kumbe zinaweza kuleta shida kwako au kwa mtoto wako tumboni.

Kuweza kuepuka mahitaji ya kutumia dawa kipindi cha ujauzito, kula mlo bora, kunywamaji ya kutosha, fanya mazoezi na pia jifunze kupumzika. Msongo wa mawazo unaweza kusababisha kila maumivu kuwa makali zaidi. Maswali yoyote kuhusu dawa ni vyema ukashirikiana na daktari wako kwani yeye ndiye mwenye uwezo na taarifa sahihi kuhusu usalama wa dawa husika na usalama wako na mtoto wako.

Dr Abduly Kisalazo

02/03/2025
Changamoto za Tezi Dume:Tezi dume ni tezi muhimu kwa afya ya mwanaume, lakini matatizo yake yanaweza kuwa na athari kubw...
02/03/2025

Changamoto za Tezi Dume:
Tezi dume ni tezi muhimu kwa afya ya mwanaume, lakini matatizo yake yanaweza kuwa na athari kubwa kwa mfumo wa mkojo na nguvu za kiume. Hali k**a Tezi Dume Kubina (Benign Prostatic Hyperplasia - BPH), Saratani ya Tezi Dume, na Prostatitis (uvimbe wa tezi dume) ni miongoni mwa changamoto zinazowakumba wanaume wengi, hasa wanapozidi kuwa na umri.

Dalili zinazojitokeza ni pamoja na ugumu wa kukojoa, kukojoa mara kwa mara, maumivu ya mgongo wa chini na kiungo cha sehemu za chini. Hali hizi ni za kawaida na zinahitaji uangalizi wa afya ili kuepuka madhara makubwa.

Address

Kimara
Dar Es Salaam
213

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr Abduly Kisalazo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share