14/05/2026
Baadhi ya dalili zinazoweza kuonyesha njia inaanza kufunguka kwa MAMA MJAMZITO ni hizi:
• Kupata Maumivu ya tumbo yanayokuja na kuondoka k**a ya hedhi, lakini yanakuwa ya mara kwa mara na kuongezeka nguvu kadri muda unavyoenda.
• Kupata Maumivu ya mgongo kwa chini, hasa yanayosambaa kuelekea tumboni au mapajani.
• Kutoka ute mzito ukeni wenye rangi ya pinki, kahawia au damu kidogo. Hii huitwa “bloody show” na hutokea baada ya ute uliokuwa umeziba mlango wa kizazi kutoka.
• Kuhisi mtoto kushuka chini zaidi kwenye nyonga. Mama anaweza kupumua vizuri zaidi lakini kwenda chooni mara kwa mara kutokana na presha ya mtoto kushuka.
• Kuhisi presha kubwa sehemu ya nyonga au uke, kana kwamba mtoto anasukuma chini.
• Tumbo kukaza mara kwa mara. Madaktari wanaeleza kuwa uchungu wa kweli huwa haupungui hata ukibadili mkao au kupumzika.
• Maji kutoka ghafla au kuvuja kidogo kidogo. Hii ni dalili muhimu inayoweza kuonyesha uchungu uko karibu au umeanza.
• Baadhi ya wajawazito hupata hali ya kuharisha, uchovu, kutetemeka au kukosa usingizi siku chache kabla ya kujifungua.
KUMBUKA;Wanawake hutofautiana pia,Kwahyo si kila mama hupata dalili zote. Wengine wanaweza kufunguka njia taratibu bila maumivu makali mwanzoni, huku wengine wakianza moja kwa moja na uchungu mkali. Pia wanawake wengine wanaweza kuwa wameanza kufunguka sentimita chache bila hata kujua mpaka Wakapimwa hospitalini.
Uzoefu wa baadhi ya akina mama ulioshirikishwa kwenye majukwaa ya wajawazito unaonyesha kuwa wengine waliona ute wenye damu, maumivu ya mgongo na presha ya nyonga saa au siku chache kabla ya kujifungua, huku wengine wakikaa wiki kadhaa wakiwa wameanza kufunguka njia bila uchungu wa kweli kuanza.
Naamini kuna kitu umepata,K**a kipo Gonga LIKE hapa........