ERY Herbal Clinic

ERY Herbal Clinic Huu ni ukurasa maalumu kwa ajili ya elimu ya tiba za magonjwa kupitia mimea | piga simu 0658505671

Ndugu yangu, jitahidi kila unapokwenda ufukweni, leta mizizi ya mnazi... Unajua kwa nini?Mzizi wa mnazi ni dawa ya jadi ...
04/06/2026

Ndugu yangu, jitahidi kila unapokwenda ufukweni, leta mizizi ya mnazi... Unajua kwa nini?

Mzizi wa mnazi ni dawa ya jadi yenye nguvu inayotumika kutibu maambukizi, kuharisha, uvimbe, matatizo ya figo, na changamoto za uzazi. Mizizi yake ina kemikali zenye uwezo wa kupambana na bakteria, virusi, na kusaidia kuondoa sumu mwilini, jambo linaloufanya kuwa sehemu yenye thamani kubwa lakini mara nyingi hupuuzwa ya mti wa mnazi.

📍Faida za Kiafya za Mizizi ya Mnazi

☑️Kutibu kuharisha na maambukizi ya tumbo — maji ya mizizi yaliyochemshwa husaidia kuua bakteria hatari na kusaidia kukaza utumbo ili kupunguza choo cha maji.

☑️Kupambana na maambukizi ya njia ya mkojo — hufanya kazi k**a kisafishaji cha asili kinachosaidia kupunguza kuungua, maumivu, na kukojoa mara kwa mara kunakosababishwa na UTI.

☑️Kupunguza uvimbe na maumivu ya mwili — husaidia kutuliza maungio yaliyovimba, arthritis, na maumivu ya misuli.

☑️Kusaidia afya ya figo — husaidia kutoa sumu mwilini na kuzuia maambukizi ya figo.

☑️Kusaidia mfumo wa uzazi wa mwanamke — hutumika kienyeji kusaidia kurekebisha hedhi na kupunguza maumivu ya hedhi.

☑️Kuongeza nguvu za kiume — mizizi ya mnazi huchemshwa pamoja na tangawizi na kunywewa k**a vi**ra ya asili

☑️Kuongeza kinga ya mwili — kemikali zake za kupambana na vijidudu husaidia kuimarisha uwezo wa mwili dhidi ya maambukizi.

☑️Kupunguza kutokwa damu ndani ya mwili (kwa hali ndogo) — maji ya mizizi yaliyochemshwa husaidia kubana mishipa ya damu na kupunguza damu kutoka.

☑️Kutibu maambukizi ya ngozi — hutumika kupaka kwenye vipele, majipu, na fangasi.

☑️Kupunguza homa — husaidia kupoza mwili na kushusha joto la mwili.

☑️Kusaidia kuondoa sumu mwilini — hudaiwa kusaidia kusafisha damu na ini kwa kuondoa taka hatari mwilini.

Hivi watu wenye mishipa inayoonekana hivi, wana sifa gani?😅
04/06/2026

Hivi watu wenye mishipa inayoonekana hivi, wana sifa gani?😅

📌JIFUNZE KITU HAPAImeandikwa na Mwl Kennedi Masawe Leo tuzungumzie kitu kinachoitwa “BRAIN ROT” yaani kuoza kwa akili ku...
04/06/2026

📌JIFUNZE KITU HAPA

Imeandikwa na Mwl Kennedi Masawe

Leo tuzungumzie kitu kinachoitwa “BRAIN ROT” yaani kuoza kwa akili kutokana na matumizi ya kupitiliza ya short videos k**a TikTok, reels na shorts.

INATOKEA VIPI

1. Unatazama video fupi fupi za ujinga - kuku anacheza mpira, mchezo wa kuigiza usio na maana, watu wanaongea upuuzi.

2. Ubongo unapata dopamine bure kila sekunde 10-15. Hii ni kemikali ya furaha.

3. Unazoea. Baada ya muda, video ya dakika 5 yenye hekima, elimu, au ushauri inaonekana “nzito kufuatilia” na “boring”.

4. Uwezo wa kuzingatia na kufikiria unadhoofika. Hata k**a unajua ni ujinga, huwezi kuacha.

DALILI ZAKE

- Hufurahi tu ukiwa na simu. Bila hiyo unachoka na kukosa raha.

- Hauwezi kusoma aya 5 bila kushika simu.

- Unajichekesha peke yako na mambo yasiyo na maana.

- Unajua ni upuuzi, lakini bado unaendelea kutazama.

Watu wengi wanachukulia k**a masihara lakini ukweli ni kwamba kuna kitu kikubwa sana kinaendelea kwenye akili za watu hasa vijana wa sasa.

Zamani mtu alikuwa anaweza kukaa chini akaangalia documentary ya dakika 30, akasoma kitabu, akafikiri maisha yake, akapanga malengo yake.

Lakini leo mpe mtu video ya dakika 5 yenye elimu utaona tayari anaanza kuchoka na kuacha kabisa kutazama video.

Lakini huyo huyo anaweza kukaa saa 4 anascroll TikTok bila hata kujua muda umeendaje 😭
Tatizo linaanzia kwenye algorithm.

Algorithm ya TikTok haijali k**a content ni ya maana au ni ujinga. Yenyewe kazi yake ni kuhakikisha huachi app.

Ndiyo maana utaona:
video za uchi
ujinga wa kuchekesha
watu wanapiga kelele
prank za kijinga
memes zisizo na maana
vinaenda sana kuliko content ya hekima au elimu.

Kwa sababu ubongo wa binadamu unapenda sana vitu vya haraka haraka. Kila swipe unapata kitu kipya.

Hii inafanya akili kupata dopamine yaani ile feeling ya furaha ya muda mfupi.

Tatizo ubongo ukizoea dopamine za haraka kila dakika, unaanza kuchukia vitu vinavyohitaji utulivu.

Yaani siku hizi 👉watu hawapendi kusoma post ndefu
👉 hawapendi kujifunza skill
👉hawapendi video ndefu yenye kuelimisha
👉hawapendi kufikiri kwa kina
👉hawapendi hata kukaa kimya dakika 10 bila simu.
Akili imezoea: “Swipe nyingine ipo nini? 😭

Hapo ndipo BRAIN ROT inaanza taratibu.

Na jambo baya zaidi watu wengi hawaoni k**a wanaathirika.
Mtu anaamka asubuhi kitu cha kwanza ni TikTok.

Anakula huku anascroll.
Anaingia chooni na simu.
Analala na reels.
Akikosa bando anakuwa k**a maisha yamesimama 😭
Hii si kawaida tena.

Akili imeanza kuwa addicted na stimulation.
Wanasaikolojia wengi duniani sasa wanaongea kuhusu kupungua kwa attention span. Yaani uwezo wa mtu ku-focus kwa muda mrefu unapungua sana.

Ndiyo maana leo mtu anaweza kusahau haraka, kuchoka haraka au kushindwa kuzingatia kazi moja kwa muda. Hata kufikiria

Na mbaya zaidi algorithm inapenda sana content ya hovyo kuliko yenye maana 😭
Utaona page inayofundisha:
biashara
maisha
maadili
elimu
hekima yenye faida utakuta ina followers 5K tu 😭😭

Lakini twende kwenye page ya upuuzi sasa👇
😭 Kunengua kiuno
😭 Udaku
😭 Kukaa utupu utakuta ina followers milioni mbili 😭

Kwa nini? 🤔
Kwa sababu content ya hovyo inatoa dopamine ya haraka kuliko content ya kujenga akili. 📌🫵

Hii ndiyo maana watu wengi sasa wanajua trends zote za TikTok lakini hawajui hata namna ya kuendesha maisha yao vizuri.

Mtu anaweza kukariri lyrics zote za nyimbo za trend lakini hawezi kukaa dakika 20 ajifunze kitu kitakachomsaidia miaka 10 ijayo.

Mitandao imezalisha “madaktari wa TikTok” 😭 yaani
Kila mtu sasa ni daktari.
Mmoja anasema: “Usile ugali.”
Mwingine: “Usinywe maji.”
Mwingine: “Kula mara moja kwa siku.”
Mwingine: “Ukila wali utakufa mapema.”

Hapo hapo anakuja mwengine anasema "Kula vyote" 🤣

Yaani full kuchanganya watu ujinga ujinga tu 😭

Wakiona mtu anaongea kwa confidence tayari wanaamini kila kitu 😭

Na algorithm ikiona watu wana-comment sana au wanabishana inaendelea kusambaza video hiyo zaidi na zaidi 😥

Ndiyo maana siku hizi ujinga unaenea faster kuliko maarifa 😭
Kuna watu mpaka hawawezi tena kukaa na mawazo yao wenyewe. Wakikaa kimya tu wanahisi boredom kali.
Lazima washike simu.

Zamani boredom ilikuwa inazalisha creativity.
Leo boredom inaua watu kwa sababu akili imezoea stimulation nonstop.

Sababu wengine 👇

huwawezi kusoma Qur’an/Bible au content yenye maneno mengi
Hawawezi kusikiliza mhadhara,
Hawawezi kufanya kazi ya muda mrefu
Akili imeharibika taratibu bila wewe kugundua

Na kitu kingine kibaya zaidi ni comparison.
Mitandao inaonyesha maisha ya uongo 😭
magari, hela, wanawake, soft life.

Mtu anaishia kuona maisha yake hayana maana na kuiga mambo kwenye mitandao 😭 video na picha nyingi ni fake 😭
Ndiyo maana anxiety na depression zimeongezeka sana kwa vijana.
Na nchi nyingine zimeanza kuhofu hali hii.

Si kwa sababu ya dance tu, bali kwa sababu wanaona vijana wengi wanapoteza focus, muda na uwezo wa kufikiri kwa kina.

Sina maana kwamba TikTok usitumie wala 😅
Tatizo ni matumizi.
Unaweza kutumia TikTok:
kujifunza biashara, editing, lugha, marketing, elimu.

Lakini ukiiacha algorithm ikuendeshe, utajikuta maisha yote ni: scroll 😂 cheka 😂 lala 😴 amka urudie tena mwisho wa siku faida hakuna 😭 Na miaka inaenda.

Mwisho wa siku ubongo unakuwa umejaa:
Nemes
Trends
Drama
Ujinga wa internet
lakini hakuna maarifa ya kweli wala maendeleo ya maisha.

Ndiyo maana siku hizi watu wengi wana taarifa nyingi kichwani… lakini hekima kidogo sana 😔
Nakusikia sana.

Hii “brain rot” unayoiona ni halisi, na inafanya kazi k**a mtego kimya kimya. 😥🫵

Kinachotokea kichwani mwako ni k**a “chakula cha haraka” kwa akili

Fikiria hivi:
Video ya kuku anayecheza mpira ni sekunde 10, inachekesha, haikutishi kufikiria chochote.

Ubongo wako unapata “dopa” - kemikali ya furaha - bure kabisa.

Video ya dakika 5 yenye hekima kuhusu maisha inahitaji akili yako ifanye kazi kidogo. Isikilize, iunganishe na maisha yako, ifikirie.

Ubongo ni mvivu kiasili. Ukimzoesha chakula cha haraka kila siku, anaanza kukataa chakula cha kawaida. Ndiyo maana “huwezi hata kuangalia video yenye manufaa”.

Hii ndiyo maana wanasaikolojia wanasema: Algorithm haiongezi IQ yako, inakufundisha kuvumilia raha rahisi tu.

Sehemu ya ubongo inayokudhibiti inachoka
Kichwani kuna sehemu inaitwa prefrontal cortex. Kazi yake ni kusema “acha, hii haina maana, fanya kitu chenye faida”.

Tafiti za MRI zinaonyesha sehemu hii inafifia kwa watu wanaotazama skrini kupita kiasi.
Inakuwa k**a gari lenye mafuta mengi lakini breki zimechoka.

Unajua ni ujinga, lakini mwili unakusukuma uendelee kuskroll.
Ndiyo maana mtu anaweza kujua “hii video ya mwanamke kunengua kiuno hainisaidii chochote”, lakini bado anaangalia dakika 40.

Unapoteza uwezo wa kufurahia mambo ya kawaida
Hapa ndipo inakuwa mbaya.
Ukipata raha kubwa kila siku kwa bure, vitu vya kawaida vinaonekana hafifu.

Kusoma hekima yako Facebook, kuzungumza na mama, kutembea jioni - vyote vinaonekana “bure”.

Hiyo ndiyo sababu mtu anasema “bila bando hana furaha” sio kwamba yeye ni mtu mbaya ni kwamba ubongo wake umezoea kiwango cha juu cha msukumo.

Wanasaikolojia wanaita hii anhedonia kutoweza kufurahia vitu ambavyo hapo awali vilikupa furaha.

Kwa nini ujinga unashika zaidi kuliko hekima?
Algorithm ya TikTok, YouTube Shorts, Reels haikuundwa kukufundisha. Imeundwa kukushika macho sekunde nyingi iwezekanavyo.

Video inayokuchanganya, kukukosea, kukuonyesha mwili, au kukufanya useme “hii ni nini?” inashikilia macho zaidi kuliko video ya dakika 5 za kujenga tabia nzuri”.

Ndiyo maana unaona page yenye wafuasi milioni 1 inaposti ujinga tu. Haileti mabadiliko, lakini inatoa raha ya sekunde 3.

Wale wenzangu na mimi sasa post kitu ambacho kina faida kwa jamii k**a ni video basi views 200 na like moja basi 😭

Pia kuna shida baadhi ya content creator wengi maudhui yao ni ujinga ujinga mwingi faida zero 😭

Ubongo haujafa umelala tu
Jambo zuri kuhusu ubongo ni kwamba unajirekebisha.

Inaitwa neuroplasticity.

K**a unavyoweza kuoza kwa kuangalia ujinga kila siku, unaweza pia kujijenga kwa kuupa akili yako chakula kizito tena.
Lakini wiki ya kwanza itakuwa ngumu.

Itakuwa k**a mtu anayeacha sukari - kila kitu kitaonekana bila ladha. Kwanini hii inatokea kwa vijana wengi?

Kwa sababu ubongo wa kijana bado unajenga.
Sehemu inayopenda raha inakomaa mapema, sehemu inayodhibiti inakomaa baadaye.
Ni k**a kuwa na gari la mbio bila breki nzuri.

Brain rot si kwamba umekuwa mjinga.

Ni kwamba umefundisha akili yako kupenda raha rahisi hadi ikashindwa kuvumilia mambo yenye maana

Lakini ukibadilisha mlo wa akili yako, hata dakika 20 kwa siku bila simu, utaanza kuhisi tofauti ndani ya wiki 2.
Be better 1% every day

K**a umejifunza kiyu nenda ukafollow ukurasa wake hivi sasa ili uendelee kupata Elimu k**a hii ya kutosha🙏

KUMSAIDIA MTOTO ANAYECHELEWA KUTEMBEA 📍Siri ya asili.Mtoto wako amechelewa sana kutembea licha ya kwamba umeona wazi na ...
04/06/2026

KUMSAIDIA MTOTO ANAYECHELEWA KUTEMBEA

📍Siri ya asili.

Mtoto wako amechelewa sana kutembea licha ya kwamba umeona wazi na hata kitabibu hana upungufu wowote wa kiafya?

Basi hii inakuhusu — Leo ninawapa suluhisho hili ambalo linaonekana la kawaida sana lakini baadaye huonekana k**a muujiza.

📍Nini cha Kufanya?
Mama mzazi wa mtoto anatakiwa avue chupi aliyolalia asubuhi mara tu anapoamka, kabla hata hajashuka kitandani au kwenye mkeka.

Kisha atumie chupi hiyo kumkanda vizuri mtoto wake kwenye maungio yote ya mwili

Kumbuka: anaweza kufanya tendo hilo akiwa nje ya kitanda au mkekani — lakini lazima avue chupi kabla hajashuka, yaani hata kabla hajakanyaga chini.

Hili lifanywe kila asubuhi kwa muda usiozidi mwezi mmoja ikiwa itaendelea.

MATOKEO:
Wakati mwingine baada ya massage ya kwanza tu, mtoto ambaye alikuwa hawezi hata kusimama huanza kukimbia ghafla. Ni muujiza wa asili!

USHAURI WETU
Je, unaweza kutumia chupi hiyo hiyo kila siku?

☑️Ndiyo, ni rahisi: ifue. Dumisha usafi. Kumbuka kwamba unatakiwa kuivua kabla hujatoka kitandani. Usifanye hivi ikiwa wewe si mama mzazi wa mtoto huyo. Mungu awe nanyi daima.

Mdharau asili hufa kikatili

Hivi huko kwenu mayai ya kuku wa kienyeji yanauzwaje?
03/06/2026

Hivi huko kwenu mayai ya kuku wa kienyeji yanauzwaje?

Nairudia tena — mti huu kisayansi hujulikana k**a “Erythrina abyssinica” maarufu k**a “lucky bean tree” — mti wa bahati,...
03/06/2026

Nairudia tena — mti huu kisayansi hujulikana k**a “Erythrina abyssinica” maarufu k**a “lucky bean tree” — mti wa bahati, wasukuma waita “nkalalywa-nkuba” ni mmea wa tiba wenye matumizi mengi katika tiba za jadi katika jamii za Afrika Mashariki, Kati na Kusini.

✅Hutumika kutibu magonjwa mbalimbali ya binadamu na mifugo, yakiwemo maambukizi ya bakteria na fangasi, kifua kikuu, malaria, VVU/UKIMWI, kuhara, saratani, meningitis, magonjwa ya uvimbe na maambukizi ya njia ya mkojo.

Mmea huu una kemikali (Phytochemicals) mbalimbali zenye matokeo ya tiba k**a vile “flavonoids”, “alkaloids”, na “terpenoids”. Zina mchango katika uwezo wa mmea huu “kuondoa uvimbe”, kupambana na bakteria, kuwa na —kinga ya mwili na kupambana na malaria.

—Flavonoids husaidia k**a vioksidishaji na hupunguza uvimbe.
—Alkaloids husaidia katika kupambana na vimelea na uvimbe pia.

Matumizi maalum ya Erythrina abyssinica k**a dawa:
—Sehemu mbalimbali za mmea huu k**a gome, mizizi, na majani hutumika kwa namna tofauti k**a vile dawa ya maji, unga au kwa kuchemshwa kulingana na aina ya tatizo.

✅Maambukizi: Hutumika kutibu maambukizi ya bakteria na fangasi, ikiwemo ya ngozi na tishu laini.
✅Malaria: Dondoo kutoka kwa mmea huu zinaonyesha uwezo wa kupambana na vimelea vya malaria.
✅VVU/UKIMWI: Baadhi ya tafiti zinaonyesha faida katika kutibu hali zinazohusiana na VVU/UKIMWI.
✅Magonjwa ya uvimbe: Hutumika kutuliza maumivu na kuponya magonjwa ya uvimbe.
✅Kuponya vidonda: Majani au gome lililosagwa huwekwa juu ya vidonda au maambukizi ya ngozi.
✅Matatizo ya tumbo: Hutumika kutibu kuhara, maumivu ya tumbo na matatizo mengine ya mfumo wa chakula.
✅Magonjwa ya kupumua: Hutumika kutibu kikohozi, bronchitis na pumu.
✅Matumizi mengine: Pia hutumika kutibu kuumwa na nyoka, magonjwa ya zinaa, uvimbe wa ini, surua na baadhi ya aina za saratani.

K**a wewe haupo kwenye group letu la Whatsap VIP ni kwamba utapitwa na mengi zinatolewa bure kwenye group.

Una mgonjwa aliyepooza?Chukua majani ya snake plantPondaponda hadi yalainike kabisaTumia kumchua (masaage) mgonjwa sehem...
03/06/2026

Una mgonjwa aliyepooza?

Chukua majani ya snake plant
Pondaponda hadi yalainike kabisa
Tumia kumchua (masaage) mgonjwa sehemu zilizopooza.

Maarifa hayana mwisho na mdharau asili hufa kikatili

Hebu k**a kuna mtu anajua anieleweshe kuhusu hizi tozo/kodi za Mazao.Ngoja nizungumzie kwa Wilaya ya MbogweKuna utaratib...
03/06/2026

Hebu k**a kuna mtu anajua anieleweshe kuhusu hizi tozo/kodi za Mazao.

Ngoja nizungumzie kwa Wilaya ya Mbogwe

Kuna utaratibu wa kulipia ushuru sijui ndiyo kodi ya mazao (wataalamu mtanisaidia). Ukiwa unatoa mazao shambani zaidi ya gunia moja unaombwa ulipie Tsh 1,500 kwa kila gunia.

Haijalishi hayo mazao unatoa shambani kwako kupeleka nyumbani, au unapeleka stoo (ghala za kuhifadhia mazao)

Usipolipia hiyo pesa inabidi mazao yako uyaache pale barrier — hili nililishuhudia mwaka juzi, mama mmoja alikuwa akitoa shambani magunia matano (5) ya mpunga kwa kutumia tela (mkokoteni wa ng'ombe)

Alipofika barrier aliombwa alipie ushuru, yule mama alisema "sina pesa" shamba langu sijawahi kuweka vibarua — ninalima mimi na watoto wangu, hata kuvuna nimevuna mwenyewe na wanangu.

Hata shamba la kulima sikukodi kwa pesa, nilielewana na mwenye shamba (mbuga) nikiivisha nitampa gunia moja la mpunga na tayari ameshachukua, na huyu mwenye mkokoteni nimeelewana naye anibebea magunia yangu nitampa debe (ndoo) moja ya mpunga.

Ikiwa nanyi hamwezi kuniacha nipite basi niwapimie ndoo moja ya mpunga mniache niende

Wale jamaa walichomjibu yule mama ni kwamba "hatuhitaji mpunga, wewe leta pesa Tsh 5000" (mwaka juzi walikuwa wanatoza 1000 kwa kila gunia). Walimwambia k**a hauna pesa uache hapa mpunga wako wote uende, siku ukipata hiyo hela njoo ulipie uchukue mpunga wako, na utalipia na hela nyingine ya ulinzi. Ukiuacha hapa mpunga wako ukalala, utalipia kila siku elfu tano ya ulinzi.

Nilipigiwa simu na mdogo wangu—ambaye ni rafiki yake na mtoto wa yule mama, akaniambia kaka hebu nisaidie elfu tano ya haraka hapa nina shida, nikamuuliza ya nini? Ndipo akanambia stori nzima ya hao watoza ushuru (mdogo wangu alikuwa miongoni mwa walioalikwa kwenda kumsaidia yule mama kuvuna mpunga) usukumani wanaita "buyobe"

Ilibidi nimtumie pesa — lakini nilibaki na maswali mengi, nikaanza kufuatilia sana juu ya hii inshu, baadhi ya watu niliojaribu kuwauliza walidai huo ni wizi tu na kwamba wao hawajawahi kulipia hiyo hela tena huwa wanapita hizo barrier na magunia yao bilashida.

Nikaja nikamuuliza mtendaji mmoja wa kijiji (VEO) akasema hiyo ni utaratibu wa kila Wilaya kwa ajili ya kujipatia mapato ya Halmashauri—na imepitishwa kuwa hivyo. K**a utataka usitozwe kodi, basi usombe mazao yako kwa kubeba gunia moja moja.

Lakini swali lilibaki palepale kwanini wengine wanatoa na wengine hawatoi? Mwaka huu ndiyo usisema kila gunia wanalipia Tsh 1,500/- kwa wenye mashamba ya mbali wamepata tabu gharama za usafiri zimekuwa juu kutokana na mafuta kupanda na bado wanatozwa ushuru/kodi.

Sasa leo katika pitapita zangu mtandaoni nikakutana na huu mjadala, nikawa nasoma baadhi ya maoni, ikaonekana hili jambo lipo sehemu nyingi hapa Tanzania, na kwakweli linaonekana kana kwamba si jambo rasmi kwa sababu mawazo ni yaleyale—baadhi hukataa kulipa na wanaachwa na wale wengine wa ndiyo mzee hulipa.

Hebu k**a kuna mtu ana uelewa na hili jambo atupe ufafanuzi zaidi—na k**a ni ukandamizwaji lifikishwe ngazi za juu, wakulima wananyonywa hakika.

Je ni sahihi mkulima anayetoa mazao shambani kupeleka nyumbani kutozwa?

Dawa ya kisukari (Diabetes type-2)—Chuma majani mabichi ya “Leucena leucocephala” pondaponda kisha chemsha—Kunywa kikomb...
03/06/2026

Dawa ya kisukari (Diabetes type-2)

—Chuma majani mabichi ya “Leucena leucocephala” pondaponda kisha chemsha
—Kunywa kikombe kimoja asubuhi na jioni
✅Tumia kwa siku 7 kisha nenda kapime sukari

Mdharau asili hufa kikatili

MAJI YA MGOMBAJe unafahamu k**a mgomba unaweza kuokoa mamilion ya pesa zako kwa ajili ya matibabu ya magonjwa sugu—yanay...
03/06/2026

MAJI YA MGOMBA

Je unafahamu k**a mgomba unaweza kuokoa mamilion ya pesa zako kwa ajili ya matibabu ya magonjwa sugu—yanayoweza kukupata wewe au ndugu zako?

🌿Shina la mgomba huwa lina maji mengi ndani yake, unaweza kulikata au kuchoma sindano na ukayapata maji yake.

💦Maji hayo ni dawa kubwa mno ya kutibu maradhi mengi, ikiwemo mawe kwenye figo.

▪️Kiufupi kila sehemu ya mgomba ni dawa; majani yake, shina lake, mizizi yake, maua na hata matunda yake.

📍Kupata elimu hii na namna ya kutumia kujitibia, unaipata ndani ya kitabu cha Rejesha afya yako bila gharama—sehemu ya pili. Ni kitabu chenye mimea 52 inayopatikana kwa urahisi katika mazingira yetu, ni mimea yenye nguvu ya kutibu magonjwa mengi

🟢Kitabu kinauzwa Tsh 10,000/- tu

Jinsi ya kufanya malipo:
Tigo (Yas) lipa: 16685956
Jina: ERY HERBAL CLINIC'

Kisha njoo whatsap, tuma screenshot ha muamala au utaje jina la account uliyofanyia malipo.

https://wa.me/255658505671

Mdharau asili hufa kikatili

Address

Geita

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ERY Herbal Clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share