TFNC Tanzania

TFNC Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from TFNC Tanzania, Nutritionist, Ilala.

TANZANIA YATOA  UZOEFU WAKE  KATIKA UFUATILIAJI WA MASUALA YA LISHE  NCHINI. Tanzania imepata fursa ya kuungana na matai...
12/05/2026

TANZANIA YATOA UZOEFU WAKE KATIKA UFUATILIAJI WA MASUALA YA LISHE NCHINI.



Tanzania imepata fursa ya kuungana na mataifa mengine 22 , kutoka katika nchi za Africa Magharibi na Kati na kutoa uzoefu wake katika kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa musuala ya lishe nchini.

Hayo yamejiri katika mkutano wa Mawaziri wa Kikanda uliofanyika nchini Togo, kuanzia tarehe 11/5/2026 na unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 13 Mei 2026, mkutano huo umeenda na kauli mbiu ya β€œWekeza katika Lishe kwa kuzingatia Miaka ya Mwanzo ya Ukuaji wa Mtoto” umehusisha nchi za Magharibi na Kati ya Afrika ambao umeandaliwa na Bank ya Dunia.

Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango ya Lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Bi. Deborah Charwe ni miongoni mwa wataalamu waliowasilisha mada katika mkutano huo ambapo amewaeleza washiriki faida ambazo Tanzania kupitia Taasisi yake ya Lishe imezipata kupitia usimamizi na utekelezaji wa Kadi Alama Jumuishi ya Lishe.

Katika mkutano huo jumla ya wajumbe 345 kutoka katika nchi 22 za Magharibi na Kati ya Africa wamehudhuria mkutano huo wenye lengo la kujadili na kuweka mikakati ya pamoja itakayosaidia kupunguza tatizo la utapiamlo kwa nchi husika.

TFNC

Advance your career with TFNC! πŸŽ“βœ¨Do you know the most effective methods for assessing dietary intake? Join us from May 1...
12/05/2026

Advance your career with TFNC! πŸŽ“βœ¨

Do you know the most effective methods for assessing dietary intake? Join us from May 18th to 21st, 2026, for our exclusive online short course.

Why should you participate?

β€’ βœ… Master modern Dietary Assessment techniques.

β€’ βœ… Earn a certificate to boost your professional profile.

β€’ βœ… Flexible learning from anywhere (Online Course).

⏳ Only six days left! Don't wait until the last minute.

πŸ“© For more information: 0717794612

🌐 Website: www.tfnc.go.tz

DietaryAssessment

K**a wewe ni mjasiriamali  unayesindika unga kwa ajili ya chakula cha watoto wenye umri miezi sita na kuendelea, Hii si ...
12/05/2026

K**a wewe ni mjasiriamali unayesindika unga kwa ajili ya chakula cha watoto wenye umri miezi sita na kuendelea, Hii si ya Kukosa

Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) imeandaa mafunzo ya muda mfupi yatakayo kusaidia kupata ujuzi wa kitaalamu katika kuongeza thamani bidhaa unayoizalisha. Mafunzo yatafanyika tatehe 20 - 21 Mei, 2026 katika ofisi za TFNC Mikocheni, Mtaa wa Sembeti.

Ada ya mafunzo ni Tsh. 160,000 tu. Jisajili sasa kwa kuskani QR kodi hapo kwenye tangazo ama tembelea:
https://www.tfnc.go.tz/announcements/kozi

Kwa maswali zaidi piga simu namba: 0681810080 au 0755249143

11/05/2026





WIZARA YA AFYA YASISITIZA UWEKEZAJI KATIKA LISHE BORAWizara ya Afya imeendelea kusisitiza umuhimu wa uwekezaji katika li...
11/05/2026

WIZARA YA AFYA YASISITIZA UWEKEZAJI KATIKA LISHE BORA

Wizara ya Afya imeendelea kusisitiza umuhimu wa uwekezaji katika lishe bora k**a sehemu ya juhudi za kuimarisha afya, maendeleo ya jamii na uchumi wa taifa. Hayo yameelezwa leo Mei 11, 2026 bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Afya Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Akiwasilisha hotuba hiyo, Waziri Mchengerwa amesema Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) imekamilisha utafiti unaobainisha gharama za athari za utapiamlo, hususan lishe pungufu hapa nchini. Matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa Tanzania inapoteza hadi asilimia 2.03 ya pato ghafi la taifa (GDP), sawa na takribani Shilingi trilioni 3.47 kwa mwaka kutokana na athari za utapiamlo katika sekta za afya, elimu na uzalishaji mali.

Aidha, Waziri Mchengerwa amesisitiza kuwa kiwango hicho ni kikwazo kwa taifa kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ya kufikia pato ghafi la Dola za Marekani trilioni 1

Amesema ni muhimu kuendelea kutekeleza mikakati madhubuti ya kupambana na lishe duni ili kupunguza upotevu huo na kujenga rasilimali watu yenye afya, uwezo na tija katika shughuli za maendeleo ya taifa.

Utafiti huo umefanyika kupitia mpango wa β€œThe Cost of Hunger in Africa (COHA)” unaoratibiwa na Umoja wa Afrika na kutekelezwa katika nchi mbalimbali za Afrika, ukiwa sehemu ya juhudi za bara la Afrika kutathmini athari za utapiamlo katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Katika uwasilishaji huo wa bajeti, viongozi mbalimbali wa taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Afya walishiriki bungeni akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna pamoja na wakurugenzi na wakuu wengine wa taasisi, wakionesha mshik**ano katika kuendelea kusukuma agenda ya afya na lishe kwa maendeleo ya taifa.

  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC)  Dkt.Germana Leyna akipokea nakala za Utafiti wa Uw...
08/05/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Dkt.Germana Leyna akipokea nakala za Utafiti wa Uwezeshwaji Wanawake na Lishe uliokuwa sehemu ya Utafiti wa Kilimo wa Mwaka 2023/24 na Utafiti wa Jinsia na Mazingira (2025), kutoka kwa Afisa Lishe Mwandamizi Bi Maria Ngilisho ambaye alikuwa miongozi mwa Wataalamu kutoka TFNC walioshiriki katika tafiti hizo.

Mei 6, 2026, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima alizindua tafiti hizo mbili za kimkakati ambazo zinatajwa Zitasaidia Serikali na wadau kupanga mipango yenye tija katika kuimarisha lishe ya jamii, kutetea usawa wa kijinsia, na kukabiliana na mabadiliko ya mazingira kwa uhakika zaidi.

sahihi ni msingi wa maendeleo
Mazingira

Leo Mei 8, 2026, Mkurugenzi Mtendaji  wa TFNC, Dkt. Germana Leyna, ameshiriki katika kipindi cha   ndani ya Bongo FM (za...
08/05/2026

Leo Mei 8, 2026, Mkurugenzi Mtendaji wa TFNC, Dkt. Germana Leyna, ameshiriki katika kipindi cha ndani ya Bongo FM (zamani TBC FM), akizungumzia mada muhimu ya β€œElimu ya Lishe Mitandaoni na Udhibiti Wake.” πŸŽ™οΈπŸ‡ΉπŸ‡Ώ

Dkt. Leyna amesisitiza kuwa katika ulimwengu wa kidijitali, ni lazima wananchi wawe makini na taarifa za lishe wanazozipata.

TFNC imeimarisha mikakati ya:

βœ… Kufuatilia na kukanusha taarifa potofu za lishe (Fact-checking).

βœ… Kutoa miongozo ya kisayansi kupitia majukwaa ya kijamii.

βœ… Kushirikiana na mamlaka za udhibiti kulinda afya ya mlaji.

πŸ₯¦πŸŽ Lishe Bora ni Msingi wa Maendeleo.

ElimuYaLishe AfyaYaJamii Tanzania

Advance your career with TFNC! πŸŽ“βœ¨Do you know the most effective methods for assessing dietary intake? Join us from May 1...
07/05/2026

Advance your career with TFNC! πŸŽ“βœ¨

Do you know the most effective methods for assessing dietary intake? Join us from May 18th to 21st, 2026, for our exclusive online short course.

Why should you participate?

β€’ βœ… Master modern Dietary Assessment techniques.

β€’ βœ… Earn a certificate to boost your professional profile.

β€’ βœ… Flexible learning from anywhere (Online Course).

⏳ Only 11 days left! Don't wait until the last minute.

πŸ“© For more information: 0717794612

🌐 Website: www.tfnc.go.tz

DietaryAssessment

πŸ“ DODOMA: Hatua nyingine kuelekea Usawa na Lishe Bora! ✨Leo, Mei 6, 2026, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake...
06/05/2026

πŸ“ DODOMA: Hatua nyingine kuelekea Usawa na Lishe Bora! ✨

Leo, Mei 6, 2026, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amezindua tafiti mbili za kimkakati:

1️⃣ Uwezeshaji wa Wanawake na Lishe (2023/24)

2️⃣ Jinsia na Mazingira (2025)

Katika hafla hiyo, Mhe. Waziri amemkabidhi nakala za matokeo hayo Afisa Lishe Mwandamizi kutoka TFNC, Bi. Maria Ngilisho kwa niaba ya Taasisi. πŸ€πŸ“œ

Kwanini Takwimu hizi ni muhimu?

Zitasaidia Serikali na wadau kupanga mipango yenye tija katika kuimarisha lishe ya jamii, kutetea usawa wa kijinsia, na kukabiliana na mabadiliko ya mazingira kwa uhakika zaidi.

Takwimu sahihi ni msingi wa maendeleo! πŸ“ˆπŸ₯¦πŸŒ

Mazingira Tanzania Dodoma

πŸ“ MIKOCHENI, DAR ES SALAAM:Ujumbe wa wataalamu wa Lishe kutoka Wizara ya Afya na Wizara ya Elimu Zanzibar, leo Mei 4, 20...
05/05/2026

πŸ“ MIKOCHENI, DAR ES SALAAM:

Ujumbe wa wataalamu wa Lishe kutoka Wizara ya Afya na Wizara ya Elimu Zanzibar, leo Mei 4, 2026, umetembelea Maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) kwa lengo la kujifunza uzoefu wa uchambuzi wa sampuli mbalimbali zinazohusiana na vyakula.

Maabara ya TFNC ni Maabara Rejea inayotambulika na kuaminika kimataifa na mashirika k**a WHO, CDC, ECSA-HS, na IGAD, ikiwa ni maabara pekee ya aina yake katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati, na Kusini. πŸ”¬πŸŒ

Ziara hii ni sehemu ya maandalizi ya utafiti wa mfumo wa ufuatiliaji wa chumvi yenye madini joto (FORTIMAS) visiwani Zanzibar, ili kuhakikisha takwimu zitakazopatikana zina vigezo vya kimataifa kwa ajili ya afya ya wananchi.

WHO CDC AfrikaMashariki ScienceAndNutrition

Imarisha taaluma yako na TFNC! πŸŽ“βœ¨Unajua mbinu bora zaidi za kutathmini ulaji wa chakula? Jiunge nasi kuanzia tarehe 18 m...
04/05/2026

Imarisha taaluma yako na TFNC! πŸŽ“βœ¨

Unajua mbinu bora zaidi za kutathmini ulaji wa chakula? Jiunge nasi kuanzia tarehe 18 mpaka 21 Mei, 2026 katika kozi yetu fupi ya mtandaoni.

Kwa nini ushiriki?

βœ… Jifunze mbinu za kisasa za kufanya tathimini ya ulaji β€œDietary Assessment”.
βœ… Pata cheti kitakachoongeza thamani katika CV yako.
βœ… Soma ukiwa popote (Online Course).

⏳ Siku 13 zimebaki! Usisubiri dakika ya mwisho.

πŸ“© Maelezo zaidi: 0717794612

🌐 Tovuti: www.tfnc.go.tz

Address

Ilala

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

0658990996

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TFNC Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category