Njombe RRH

Njombe RRH Ukurasa Rasmi wa Hospitali ya
Rufaa Mkoa wa Njombe
59017 Ramadhani -Njombe
P. O Box 1044 Njombe

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Bi. Kuruthum Sadick ametoa wito kwa wauguzi wote Hlamashauri ya Mji wa Njomb...
12/05/2026

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Bi. Kuruthum Sadick ametoa wito kwa wauguzi wote Hlamashauri ya Mji wa Njombe kutanguliza utu na huduma bora kwa wananchi ili kutimiliza sifa ya wito kwa kada hiyo.

Ametoa kauli hiyo katika kilele cha Maadhimisho ya wiki ya Wauguzi duniani leo Mei 12, 2026, ambayo imefanyika katika viwanja vya Stendi ya zamani ya Halmashauri ya Mji Njombe.

Bi. Kuruthum amesema kuwa Uwekezaji katika vifaa na ongezeko la Ajira za Uuguzi uliofanywa na serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan umechagiza kwa kiasi kikubwa kupunguza simu za Malalamiko ya wananchi na hivyo akatoa wito kwa watumishi wa kada hiyo kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuunga mkono juhudi hizo za Mhe. Rais.

Naye Mganga Mkuu, Halmashauri ya Mji Njombe, Dkt. Jabil Juma, amesema ipo haja kubwa ya wauguzi kuelewa kuwa waajiri wao ni wananchi, hivyo kuenenda kinyume na utumishi wao inaweza kuzorotesha Afya ya wananchi, ulemavu wa kudumu hadi kifo; kwa kauli hiyo akawataka kuendelea kutoa huduma za kuridhisha ili kuendelea kuwahamasisha wananchi kurudi na kupata huduma katika vituo vyao vya kutolea huduma.

Maandamano ya Amani ya Siku ya Wauguzi Duniani katika Halmashauri ya Mji Njombe, yalitanguliwa na kuwatembelea wagonjwa waliolazwa katika kituo cha Afya cha Kanisa la Anglican kilichopo, Chaugingi, Halmashauri ya Mji Njombe, kisha baadae kuelekea Viwanja vya Stendi ya Zamani, ambapo zilifanyika shughuli mbalimbali, ikiwemo Sanaa ya Maigizo yenye lengo la kutoa ujumbe kwa jamii kuhusu huduma za Uuguzi.

Tunawatakia Wauguzi wote Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe na kote Duniani, Maadhimisho mema ya siku hii muhimu kwao.
12/05/2026

Tunawatakia Wauguzi wote Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe na kote Duniani, Maadhimisho mema ya siku hii muhimu kwao.

11/05/2026

Wizara ya Afya inatarajia kuongeza wigo katika eneo la Huduma za kibingwa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa kutoka Huduma 11 zilizopo sasa hadi huduma 17 katika mwaka wa Fedha 2026/2027.

Hayo yamesemwa leo Mei 11, 2026 na Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa katika Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya iliyowasilishwa Bungeni jijini Dodoma.

Wizara ya Afya imeliomba Bunge kupitisha kiasi cha Tsh. Trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027

11/05/2026
11/05/2026

Umuhimu wa kuhudhuria Kliniki wakati wa Ujauzito.

11/05/2026

Kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Wauguzi Duniani ambayo ni kesho Mei, 12.

Muuguzi, Faraja Mwahayola kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe anatupitisha katika kuifahamu Historia ya Uuguzi na Ukunga nchini Tanzania, kabla ya Ukoloni, kipindi cha Ukoloni na baada ya Uhuru.

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiwasili katika viwanja vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dod...
11/05/2026

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiwasili katika viwanja vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma leo Mei 11, 2026 kwa ajili ya kuwasilisha Bajeti ya Wizara ya Afya Fungu 52 kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Bajeti hiyo imezingatia uimarishaji wa huduma za afya nchini kupitia vipaumbele kumi na kimoja vya kimkakati vinavyolenga kuboresha huduma kwa wananchi.

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kusomwa leo Mei 11 Bungeni jijini Dodoma
11/05/2026

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kusomwa leo Mei 11 Bungeni jijini Dodoma

Nyote Mnakaribishwa
10/05/2026

Nyote Mnakaribishwa

Address

Mgodechi/Ramadhani Njombe Mjini
Njombe
59107

Telephone

+255678888654

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njombe RRH posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Njombe RRH:

Share