24/04/2026
Hivi kitaalamu vinaitwa Tonsil Stones. Vinatokana na mabaki ya chakula, seli zilizokufa, na ute (mucus) kunasa kwenye matundu ya tezi za koo (tonsils). Baada ya muda, uchafu huo unajikusanya na kuwa migumu k**a vijiwe. Mara nyingi husababisha koo kuwasha na harufu mbaya mdomoni.
NJIA YA KUZUIA HALI HII
Kwa hatua za awali, njia rahisi ni kusukutua kwa nguvu kwa kutumia maji ya uvuguvugu yaliyochanganywa na chumvi (Saline Gargle) ili kusaidia kulegeza vijiwe vilivyojiunda. Pia, wengine hutumia vifaa laini k**a cotton swabs kuviondoa kwa umakini bila kuumiza tishu za koo.
​Kitaalamu, k**a tatizo ni sugu na linajirudia, tiba ya kudumu ni Tonsillotomy au Tonsillectomy (upasuaji mdogo wa kuondoa tezi za koo). Pia kuna teknolojia ya kisasa ya Laser Tonsil Cryptolysis, ambayo hutumia leza kuziba yale matundu (crypts) ili kuzuia uchafu usinase tena. Kikubwa ni kuzingatia usafi wa kinywa ili kudhibiti mrundikano wa bakteria na seli zilizokufa."
Dr Bwire healthy services Your healthy our priority 😀